HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 27 December 2013

MKUU WA MKOA WA TANGA AWAONYA MADEREVA MWENDO KASI HASA MSIMU HUU WA SIKUKUU


Mkuu wa Mkoa wa Tanga Chiku Gallawa

Na Oscar Assenga, Muheza.
MKUU wa Mkoa wa Tanga, Luteni Mstaafu Chiku Gallawa amewataka madereva mkoani Tanga kuhakikisha wanajiepusha na ajali barabarani kwa kutoendesha mwendo kasi hasa katika kipindi hiki cha sikukuu za mwishoni mwa mwaka.
Mkuu wa Mkoa akikabidhi Misaada hiyo

Gallawa alitoa kauli hiyo juzi wilayani hapa wakati akizungumza wananchi wa mkoa wa Tanga mara baada ya makabidhiano ya zawadi za krismas zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete katika makazi ya wazee wasiojiweza misufini kata ya Ngomeni wilayani hapa.
 
Alisema kuwa mara nyingi wakati wa sikukuu na mwishoni mwa mwaka madereva wengi wamekuwa wakiendesha magari yao kwa mwendo kasi bila kujali kuwa wanaweza kukumbana na ajali na kupoteza maisha ya watu pamoja na kuleta simazi kwa Taifa.
Misaada iliyotolewa
 “Nasisitiza madereva acheni kuendesha magari mwendo kasi kwani bado tuna majonzi ya ajali zilizotokea ndani ya mwaka huu na kusababisha maisha ya raia wasio na hatia kukatizwa huku wengine wakibaki na ulemavu wa kudumu “Alisema Gallawa.

Katika hatua nyengine, Gallawa aliwataka wananchi wa mkoa wa Tanga kudumisha utulivu na amani kwa kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani na kuwa mstari wa mbele kutoa taarifa kwa vyombo husika kwa viashiria vya kutoweka kwa amani.

Hata hivyo mkuu wa mkoa huyo alisisitiza suala la usafi katika maeneo mbalimbali jijini hapa kwa kuwataka wananchi kuendelea kuyaweka mazingira yao katika muonekano mzuri kwa wageni na wenyeji.

Katika makadbidhiano hayo, Mkuu huyi wa mkoa alikabidhi zawadi zilizotoka kwa Mh.Rais mchele Kilo 150, mbuzi watatu(3),na mafuta ya chakula lita 40,miche mitano ya sabuni pamoja na katoni moja ya chumvi vyote vikiwa na thamani ya fedha taslimu sh.615,000.

Wakati huo huo,Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga limesema hakuna matukio matukio makubwa yaliyojitokeza katika kusheherekea sikukuu ya krismas iliyoazimishwa jana katika maeneo mbalimbali nchini.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga,Kamishna Msaidizi wa Polisi ,Constatine Massawe alisema jeshi  la polisi mkoani hapa limejipanga vizuri katika kukabiliana na matukio yoyote ya kiuhalifu ambayo yanaweza kujitokeza katika kipindi hiki cha sikukuu na mwisho wa mwaka.

No comments:

Post a Comment