HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 20 November 2013

"UHAI CUP" AZAM FC WAICHAPA YANGA 2-0 CHAMAZI, MTIBWA SUGAR, ASHANTI NAZO ZATAMBA



Bench la Ufundi la Azam fc
AZAM FC imeendeleza wimbi la ushindi katika michuano ya timu za vijana za klabu za Ligi Kuu ya Bara chini ya umri wa miaka 20, maarufu kama Kombe la Uhai, baada ya kuilaza mabao 2-0 Yanga SC, Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam jioni ya leo.
Mabao ya Azam leo yamefungwa na Adam Omar dakika ya saba na Gadiel Michael dakika ya 39.
Katika mchezo mwingine uliofanyika Uwanja wa Karume, Ilala, Dar es Salaam jioni hii, bao pekee la Patrick Mdidi dakika ya 38 limetosha kuipa Mtibwa Sugar ushindi wa 1-0 dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora.


Katika mechi za asubuhi, Ashanti United iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya JKT Oljoro ya Arusha Uwanja wa Azam Complex. Mabao yote ya Ashanti yalifungwa na mtoto wa beki wa zamani wa kimataifa Tanzania na klabu ya Yanga, Salum Kabunda ‘Ninja Msudan’ (marehemu), aitwaye Ally Salum Kabunda anayecheza na mdogo wake, Hassan Salum Kabunda pia katika timu hiyo na wote wafungaji wazuri.

Uwanja wa Karume, Kagera Sugar iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Prisons ya Mbeya, mabao ya Mohammed Mohammed na Hassan Rajab, wakati Uwanja wa DUCE, Mbeya City iliifunga 1-0 JKT Ruvu na Ruvu Shooting ikatoka sare ya 1-1 na Mgambo JKT.

No comments:

Post a Comment