HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 19 November 2013

MSIMBAZI KWAWAKA MOTO, VIONGOZI WATIMUANA KAZI, WENGINE WAJIZOLEA VYEO VYA UBWECHE



Rage
Kuhusu Rage
Aliyekuwa akikaimu nafasi ya Umakamu uenyekiti wa Simba, Joseph Itang’are ‘Mzee Kinesi sasa ndiye mwenyekiti mpya Simba.

Itang’are alikuwa akikaiumu nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Kaburu aliyeamua kuachia ngazi.Sasa ndiye atakuwa mwenyekiti mpya wa Simba, saa chache tu baada ya mwenyekiti, Ismail Aden Rage kusimamishwa.

Mmoja ya wajumbe wa kamati ya utendaji, Swed Nkwabi yeye ameteuliwa kuwa kaimu makamu mwenyekiti.
Mzee Kinesi (kushoto)akiwa na Julio(katikati) na Kibaden(kulia)
KUHUSU KIBADEN
Baada ya kuwatimua makocha wake, Abdallah Kibadeni na msaidizi wake, Jamhuri Kiwhelo ‘Julio’, Simba sasa imemchukua kocha Zdravko Logarusic raia wa Croatia.

Tayari Simba imemaliza mazungumza na kocha huyo na anatarajia kutua nchini hivi karibuni kwa ajili ya kusaini mkataba na mara moja kuanza kazi.

Kabla ya hapo, Logarusic alikuwa kocha wa Gor Mahia ya Kenya aliyoifundisha kwa misimu miwili akisha nafasi ya pili.

Msimu huu ulikuwa wa mwisho, lakini aliondoka katikati na nafasi yake kuchukuliwa na Bobby Williamson ambaye baadhi ya vyombo vya habari viliripoti anajiunga na Simba, kitu ambacho hakikuwa sahihi.
Baadaye Bobby alikanusha kuwa amefanya mazungumzo na Simba na ataendelea kubaki Kenya.

Selemani Matola
KUHUSU JULIO
SULEIMAN Abdallah Matola sasa anakuwa Kaimu Kocha wa Simba SC baada ya makocha wote, Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibadeni’ na Msaidizi wake Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ kusimamishwa.

Matola ambaye kwa sasa ni Kocha Mkuu wa Simba B, atakuwa Kocha Msaidizi wa kocha mpya wa kigeni, atakayetambulishwa Desemba 1, mwaka huu.


Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Simba SC, Joseph Itang’are ‘Kinesi’ amewaambia Waandishi wa Habari leo mchana makao makuu ya klabu, Mtaa wa Msimbazi kwamba, pamoja na kuwasimamisha makocha hao kwa kutoridhishwa na uwezo wao, pia wamemsimamisha Mwenyekiti, Alhaj Ismail Aden Rage kwa madai hawana imani naye.

Kinesi alisema uamuzi huo ulifikiwa katika kikao cha Kamati ya Utendaji kilichofanyika jana Dar es Salaam.
Kinesi amesema sasa yeye ndiye atakaimu Nafasi ya Uenyekiti wa klabu hadi hapo Mkutano Mkuu utakapofanyika.

Ikumbukwe Kinesi alichaguliwa kama Mjumbe tu wa Kamati ya Utendaji na Makamu Mwenyekiti ni nafasi ambayo anakaimu baada ya kujiuzulu kwa Geoffrey Nyange ‘Kaburu’. 
Hata hivyo, Rage hakuwepo kwenye kikao cha Kamati ya Utendaji jana na Kinesi alipoulizwa alisema kiongozi huyo yupo safarini.

No comments:

Post a Comment