HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Saturday, 9 November 2013

TANZANITE YAPIGA MTU 15-1




Kikosi Cha The Tanzanite


Timu ya Taifa ya Wanawake wenye umri chini ya miaka 20 The Tanzanite imechaibanga Timu ya Wenzao ya Taifa ya Msumbiji kwa Jumla ya mabao 15-1 baada ya kupata ushindi mwingine mnono wa mabao 5-1 katika mchezo uliochezwa hii leo katika Dimba la Zimpeto jijini Maputo nchini Msumbiji.

Mabao ya The Tanzanite leo yamewekwa kimiani na Selda Boniface aliefunga matatu “hart trik” Vumilia Maarifa na Dionosian Maarifa aliofunga bao 1 kila mmoja.

Timu hiyo ya Msumbiji imetolewa kwa jumla ya magoli 15-1 baada ya kufungwa kipigo cha 10-0 walichokipata wakiwa ugenini nchini Tanzania wiki 2 zilizo pita na cha 5-1 walichokipata leo wakiwa nyumbani kwao nchini Msumbiji.

Kwa matokeo hayo Tanzanite wanasubiri mshindi kati ya Botswana na Africa ya Kusini ambapo wakishinda wataingia rasmi kwenye kinyang’anyiro cha kuwania kombela Dunia nchini CANADA.

No comments:

Post a Comment