HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Saturday, 9 November 2013

TAARIFA ZA LIGI KIMATAIFA BARCLAYS,LA LIGA,BUNDES LIGA NA SERIA A


BUNDESLIGA: MABINGWA BAYERN, LEVERKUSEN SAFI, DORTMUND HOI! 

MABINGWA Watetezi wa Bundesliga huko Germanny, Bayern Munich, leo wameendeleza ushindi huku wapinzani wao wa karibu Borussia Dortmund kufungwa lakini Bayer Leverkusen kupata ushindi mnono.
 
Frank Ribery

Bayern waliichapa FC Augsburg Bao 3-0 kwa Bao za Jerome Boateng, Franck Ribery na Penati ya Thomas Muller.
Nao Borussia Dortmund, waliokuwa Ugenini, walitangulia kufunga Bao katika ya 45 kwa Bao la Marco Reus lakini VfL Wolfsburg walizinduka na kupiga Bao 2 katika Dakika ya 56, Mfungaji akiwa Rodriguez na Dakika ya 69 kwa Bao la Olic na kuibwaga Dortmund Bao 2-1.

Bayer Leverkusen waliicharaza Hamburger huku Son Heung-Min akipiga Hetitriki na Bao zao nyingine kufungwa na Stefan Kiessling na Gonzalo Castro.
Bao za Hamburger zilifungwa na Beister na Pierre-Michel Lasogga, Bao mbili.

MSIMAMO-Timu za Juu
[Kila Timu imecheza Mechi 12]
-Bayern Munich Pointi 32
-BV Borussia Dortmund 28
-Bayer 04 Leverkusen 28
-VfL Wolfsburg 21
-Schalke 20

RATIBA/MATOKEO
Jumamosi Novemba 9
Bayer 04 Leverkusen 5 Hamburger SV 3
Bayern Munich 3 FC Augsburg 0
Schalke 3 SV Werder Bremen 1
VfL Wolfsburg 2 BV Borussia Dortmund 1
TSG Hoffenheim 2 Hertha Berlin 3
2030 Borussia Mönchengladbach  FC Nuremberg
Jumapili Novemba 10
1730 FSV Mainz v Eintracht Frankfurt
1930 SC Freiburg v VfB Stuttgart

LA LIGA
 


RONALDO APIGA HETITRIKI, REAL YAFUMUA 5-1!!

Cristiano Ronaldo hapo jana amepata Hetitriki yake ya 23 kwa Real Madrid wakati Klabu yake hiyoilipoitwanga Real Sociedad Bao 5-1 kwenye Mechi ya La Liga. 

Ronaldo ndie aliefunga Bao la kwanza kabla kumlisha Karim Benzema kufunga Bao la Pili na kufuatia Penati aliyofunga Ronaldo Bao la 3 kwa Real.
++++++++++++++++++

MAGOLI:
Real Madrid 5
-Ronaldo Dakika ya 12, 26 (Penati), & 76
-Benzema 18
-Khedira 36
Real Sociedad 1
-Griezmann 61

++++++++++++++++++
Gareth Bale akamtengenezea Sami Khedira kupiga Bao la 4 na Real Sociedad wakapata Bao lao moja Mfungaji akiwa Antoine Griezmann.
Ronaldo alifunga Bao lake la 3 kwenye Mechi hii na la 5 kwa Real kwa frikiki safi.
Ushindi huu umewafanya Real, walio Nafasi ya 3 na wakiwa wamecheza Mechi moja zaidi, kufikisha Pointi 31 na mbele yao wapo Atletico Madrid wenye Pointi 33 na Barcelona Pointi 34.



RATIBA/MATOKEO:
[Saa za Bongo]
Ijumaa Novemba 8
Granada CF 3 Malaga CF 1
Osasuna 0 Almeria 1
Jumamosi Novemba 9
Real Madrid 5 CF Real Sociedad 1
2000 Getafe v Elche
2200 Athletic de Bilbao v Levante
0000 Celta de Vigo v Rayo Vallecano
Jumapili Novemba 10
1400 RCD Espanyol v Sevilla FC
1900 Valencia v Real Valladolid
2100 Villarreal v Atletico de Madrid
2300 Real Betis v FC Barcelona

LIGI KUU ENGLAND
 

PENALTI TATA YAIOKOA CHELSEA, LIVERPOOL YABAMIZA!

+++++++++++++++++++++++

RATIBA/MATOKEO:
[Saa za Bongo]
Jumamosi Novemba 9
Aston Villa 2 Cardiff 0
Chelsea 2 West Brom 2
Crystal Palace 0 Everton 0
Liverpool 4 Fulham 0
Southampton 4 Hull City 1
20:30 Norwich v West Ham
++++++++++++++++++++++++ 

ASTON VILLA 2 CARDIFF 0
Frikiki ya Leandro Bacuna katika Dakika ya 76 na kichwa cha Dakika ya 84 cha Libor Kozak leo kimemaliza Masaa 7 na Nusu bila kutingisha wavu na kuwapa Aston Villa ushindi wa Bao 2-0 Uwanjani kwao Villa Park walipoifunga Cardiff City.
VIKOSI:
Aston Villa: Guzan, Bacuna, Vlaar, Clark, Baker, El Ahmadi, Westwood, Sylla, Tonev, Benteke, Kozak
Cardiff: Marshall, Taylor, Caulker, Turner, Whittingham, Medel, Odemwingie, Gunnarsson, Cowie, Theophile-Catherine, Bellamy.

++++++++++++++++++++++++

CHELSEA 2 WEST BROM 2
Leo Uwanjani kwao Stamford Bridge, Chelsea itabidi wamshukuru Refa Andre Marriner kwa kuwaokoa toka kwenye kipigo baada ya kuwapa Penati tata katika Dakika ya 93 wakati West Brom wanaongoza Bao 2-1.
Penati hiyo ilitolewa na Refa huyo baada ya Mchezaji wa Chelsea Ramires kuanguka baada kugongana na Steven Reid na Penati hiyo kufungwa na Eden Hazard.
Samuel Etoo

Chelsea ndio walitangulia kufunga katika Dakika ya 45 kwa Bao la Samuel Eto'o lakini Kipindi cha Pili West Brom wakafunga Bao mbili kupitia Shane Long Dakika ya 60 na Stephane Sessegnon Dakika ya 68.
Baada Dakika 90 kwisha Bango likaonyesha Dakika 4 za nyongeza na ndipo Dakika ya 93 ikaja Penati tata iliyolinda Rekodi ya Jose Mourinho ya kutofungwa Nyumbani kwenye Ligi.
VIKOSI:
Chelsea: Cech; Ivanovic, Cahill, Terry, Azpilicueta; Ramires, Lampard; Hazard, Oscar, Willian; Eto'o
West Brom: Myhill; Reid, McAuley, Olsson, Ridgewell; Yacob, Mulumbu; Amalfitano, Sessegnon, Brunt; Long

++++++++++++++++++++++++

CRYSTAL PALACE 0 EVERTON 0
Crystal Palace leo wamepata Pointi yao ya kwanza katika Mechi 8 za Ligi walipotoka Sare ya 0-0 na Everton.
VIKOSI:
Crystal Palace: Speroni, Ward, Gabbidon, Delaney, Moxey, Jedinak, Dikgacoi, Bannan, Thomas, Bolasie, Chamakh
Everton: Howard, Coleman, Jagielka, Distin, Baines, McCarthy, Barry, Mirallas, Osman, Pienaar, Lukaku

++++++++++++++++++++++++

LIVERPOOL 4 FULHAM 0
Wakiwa kwao Anfield, Liverpool wameifumua Fulham Bao 4-0 kwa Bao za Fernando Amorebieta, kwa kujifunga mwenyewe, Martin Skrtel  na Bao mbili za Luis Suárez.
Ushindi huu umeifanya Liverpool wakamate Nafasi ya Pili wakiwa Pointi 2 nyuma ya Arsenal.
VIKOSI:
Liverpool: Mignolet, Johnson, Skrtel, Agger, Cissokho, Lucas, Gerrard, Henderson, Coutinho, Suarez, Sturridge
Fulham: Stekelenburg, Zverotic, Senderos, Amorebieta, Richardson, Dejagah, Parker, Sidwell, Kacaniklic, Kasami, Berbatov

++++++++++++++++++++++++

SOUTHAMPTON 4 HULL 1
Southampton leo wameendeleza matokeo mazuri kwa Timu yao Msimu huu kwa kuichapa Hull City Bao 4-1.
Bao za Southamton zilifungwa na Morgan Schneiderlin, Rickie Lambert, kwa Penati, Adam Lallana na Steven Davis.
Bao la Hull City lilifungwa na Yannick Sagbo.
VIKOSI:
Southampton: Boruc, Clyne, Fonte, Lovren, Shaw, Wanyama, Schneiderlin, Ward-Prowse, Lallana, Rodriguez, Lambert
Hull City: Harper, Rosenior, Figueroa, Davies, McShane, Elmohamady, Boyd, Meyler, Huddlestone, Livermore, Sagbo

++++++++++++++++++++++++ 


RATIBA
[Saa za Bongo]
Jumapili Novemba 10
15:00 Tottenham v Newcastle
17:05 Sunderland v Man City
19:10 Man United v Arsenal
19:10 Swansea v Stoke
++++++++++++++++++++++++
 

SERIE A: LEO JUMAPILI NI JUVENTUS v NAPOLI!! 

 

>>VINARA AS ROMA KUCHEZA NA TIMU YA MKIANI SASSUOLO CALCIO!
Jumapili huko Italy kwenye SERIE A, Mabingwa wa Italy Juventus watawakaribisha Napoli kwenye pambano ambalo zinazikutanisha zilizo Nafasi za Pili na za Tatu kwenye Ligi, zote zikiwa na Pointi sawa, Pointi 28, ambazo ni 3 nyuma ya Vinara AS Roma.
Napoli wanakamata Nafasi ya Pili mbele ya Juventus kwa sababu ya ubora wa Magoli.

++++++++++++++++++++

SERIE A

MSIMAMO-Timu za Juu:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
AS Roma
11
10
1
0
25
2
23
31
2
SSC Napoli
11
9
1
1
24
8
16
28
3
Juventus FC
11
9
1
1
23
10
13
28
4
Inter Milan
11
6
4
1
27
12
15
22
5
Hellas Verona
11
7
1
3
22
17
5
22
6
ACF Fiorentina
11
6
3
2
22
13
9
21

++++++++++++++++++++

Wakati pambano hilo kali likichezwa Juventus Stadium, Vinara AS Roma watakuwa Nyumbani kucheza na US Sassuolo Calcio ambao wako Nafasi ya 3 toka mkiani wakiwa na Pointi 9 tu.
Juve na Napoli zinatinga kwenye Mechi hii zikitoka kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI ambako Juve walitoka Sare ya 2-2 na Real Madrid na Napoli kuifunga Marseille Ba0 3-2.
Kwenye Serie A, Napoli, chini ya Kocha Rafael Benitez, na Juve, chini ya Antonio Conte, zote zipo kwenye wimbi la kushinda Mechi 3 mfululizo.

Juve watatinga kwenye mtanange huu na Napoli bila ya Stephan Lichtsteiner, Mirko Vucinic na Simone Pepe ambao ni majeruhi.
Napoli, ambao watakuwa na Kikosi kamili, watawategemea zaidi Jose Callejon, Marek Hamsik na Gonzalo Higuaian kuwapa ushindi lakini huko Turin ambako wamekutana mara 67 na Juve, Napoli wameshinda mara 7 tu na kufungwa mara 40 kikiwemo kipigo cha 2-0 Msimu uliopita.

VIKOSI VINATARAJIWA:
Juventus: Buffon; Barzagli, Bonucci, Chiellini; Isla, Vidal, Pirlo, Pogba, Asamoah; Quagliarella, Tevez
Napoli: Reina; Maggio, Fernandez, Cannavaro, Armero; Inler, Behrami; Callejon, Hamsik, Mertens; Higuain

SERIE A

RATIBA:
[Saa za Bongo]
Jumamosi Novemba 9
2000 Calcio Catania v Udinese Calci
2245 Inter Milan v AS Livorno Calcio
Jumapili Novemba 10
1430 Genoa v Hellas Verona FC
1700 Atalanta v Bologna FC
1700 AC Chievo Verona v AC Milan
1700 Parma v SS Lazio
1700 AS Roma v US Sassuolo Calcio
1700 Cagliari Calcio v Torino FC
2245 Juventus v SSC Napoli
2245 ACF Fiorentina v UC Sampdoria

NANI BINGWA AFRIKA, AL AHLY AU ORLANDO PIRATES?? 

 

JUMAPILI Usiku huko Cairo Nchini Egypt Klabu Bingwa ya Afrika itapatikana baada ya Mechi ya Marudiano ya Fainali ya CAF CHAMPIONZ LIGI kati ya Mabingwa Watetezi Al Ahly ya Egypt na Orlando Pirates ya Afrika Kusini huku Al Ahly wakiwa na hazina ya Bao la Ugenini kwani Timu hizi zilitoka Sare ya Bo 1-1 huko Johannesburg Wiki iliyopita.

Katika Mechi hiyo ya kwanza Al Ahly walitangulia kufunga kwa Bao la frikiki ya Mkongwe Mohamed Aboutrika katika Dakika ya 14 na Pirates kusawazisha kwa Bao la mwishoni la Dakika za Majeruhi la Thabo Matlaba.
 
Thabo Matlaba

Timu hizi pia zilikuwa kwenye Kundi moja kwenye Mashindano haya na Pirates kuifunga Al Ahly 3-0 huko Egypt kwenye Mechi ambayo walidai kipigo hicho ni kwa sababu walikuwa kwenye Mfungo wa Ramadhani.

Katika Marudiano huko Johannesburg, Pirates na Al Ahly zilitoka 0-0 na zote hizi kufuzu kuingia Nusu Fainali.

Kwenye Nusu Fainali, Pirates waliibwaga Esperance ya Tunisia kwa Bao la Ugenini baada kutoka 0-0 huko Johannesburg na 1-1 huko Tunis.

Nao Al Ahly walitoka 1-1 na Coton Sport ya Cameroun katika Mechi zao zote mbili na Al Ahly kutinga Fainali kwa Mikwaju ya Penati 7-6.

Wakati Orlando Pirates wametwaa CAF CHAMPIONZ LIGI mara 1 tu, Mwaka 1995, Al Ahly washabeba Ubingwa huu mara 7.
Mechi hii ya Marudiano itaanza Saa 1 Usiku kwa Saa za Bongo na kurushwa moja kwa moja na Kituo cha TV cha SuperSport.

No comments:

Post a Comment