HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Saturday, 16 November 2013

TANGAZO "MGAO WA UMEME KUANZA TENA KWA BAADHI YA MIKOA NCHINI"



 
BADRA MASOUD

SHIRIKA la Umeme la Tanzania (TANESCO), limetangaza kuwapo kwa upungufu wa umeme katika mikoa yote inayotegemea gridi ya taifa kuanzia leo.
Mikoa itakayoathirika  na tatizo hilo ni Pwani, Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Dodoma, Morogoro, Singida, Mbeya, Manyara, Zanzibar, Shinyanga na Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Meneja Uhusiano wa TANESCO, Badra Masoud, alisema upungufu  huo wa umeme utadumu hadi Novemba  26 mwaka huu.
Alisema kila mkoa utakosa umeme kwa muda wa saa mbili kwa siku kwa nyakati tofauti.
Masoud alisema tatizo hilo linatokana na upungufu wa gesi kutoka katika kituo cha Songosongo kilichoko wilaya ya Kilwa, mkoa wa Lindi, unaosababishwa na matengenezo ya kiufundi kwenye visima vya gesi unaofanywa na kampuni ya Pan Afrika.
“Matengenezo ni muhimu hayaepukiki, lengo la matengenezo hayo ni kuboresha upatikanaji wa gesi ya kutosha kwenye visima hivyo,” alisema.


No comments:

Post a Comment