HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 8 November 2013

TAMAA YA FEDHA YAMFUKUZISHA KAZI WAZIRI WA MAWASILIANO WA GHANA




Naibu waziri wa mawasiliano nchini Ghana Victoria Hammah ameachishwa kazi baada ya kunukuliwa akisema kuwa atasalia katika siasa hadi atakapo pata fedha kiasi cha dola milioni moja.
Victoria Hammah

Anaonekana katika kanda ya video akisema kuwa ukiwa na pesa unaweza kuwashawishi watu. Bi Hammah bado hajatoa tamko lolote kuhusiana na mkanda huo wa video au hatua ya kufutwa kazi.
Mwandishi wa BBC mjini Accra anasema Bi Hammah alikuwa na ushawishi mkubwa katika uchaguzi wa rais John Mahama mwaka jana.

Baada ya uteuzi wake baadhi ya wadadisi walionya kuwa ana umri mdogo sana kuweza kuhudumu katika serikali.Mwezi Agosti alinukuliwa akisema kuwa kuna shinikizo za kumtaka aibe fedha za umma kwa kuwa watu hudhani kwamba yeye ni tajiri kwa sababu ya wadhifa wake wa uwaziri.

Katika kanda hiyo alisikika akisema kuwa hatatoka katika siasa hadi atakapopata dola milioni moja.Pia alisikika akimkosoa waziri mwenzake akisema hana akili,ana sura mbaya na anapenda sana kujigamba na kuwafokea watu.

No comments:

Post a Comment