HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 8 November 2013

M23 WACHOSHWA NA KIPIGO SASA WAKUBALI YAISHE



Makubaliano kusainiwa Jumatatu Kampala


Jamhuri  ya  Kidemokrasi  ya  Kongo  itatia  saini makubaliano  ya  amani siku  ya  Jumatatu  na  kundi  la waasi  la  M23 baada  ya  kundi  hilo  kuweka  silaha zao chini  wiki  hii kufuatia  kushindwa   katika  mapambano. 


Waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Kongo, Raymond Tshabanda,  ameliambia  shirika  la  habari  la  Reuters  leo kuwa  imeamuliwa  siku  moja  baada  ya  kundi  la  M23 kutangaza  kuachana  na  uasi  wao  kuwa  serikali  itawapa siku  tano  kabla  ya  kutia  saini.

 Akiwa  katika  ziara  nchini Ufaransa,  Tshabanda  amesema  kuwa  utiaji  saini  ni muhimu  kwa sababu  unalenga  kuwaingiza  wapiganaji wa  M23  katika  makambi  ya  jeshi  la  nchi  hiyo  na kulivunja  kabisa  kundi  hilo  pamoja  na  kutatua  matatizo mengine.

No comments:

Post a Comment