HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 20 November 2013

RAGE AANDAA BONGE LA SINEMA SIMBA SC KUJIBU MAPIGO YA AKINA KINESI…MCHEZO UTAANZA IJUMAA ATAKAPOTUA AIRPORT


Mzee Kinesi



MWENYEKITI aliyesimamishwa Simba SC, Alhaj Ismail Aden Rage atarejea nchini Ijumaa na kulakiwa na mamia ya wanachama na ataitisha Mkutano Mkuu, ambao utafanyika Jumapili hii.

Na katika Mkutano huo, Rage amepanga kuwasimamisha Wajumbe wote wa Kamati ya Utendaji na baada ya hapo atasafiri kwenda nje ya nchi. Wajumbe wa Kamati ya Utendaji waliobaki Simba SC ni Joseph Itang’are ‘Kinesi’, Said Pamba, Ibrahim Masoud ‘Maestro’, Swedi Nkwabi na Zacharia Hans Poppe. 

Habari zimesema kwamba, Rage amekwishawasiliana na wafuasi wake wa Dar es Salaam na wameandaa mapokezi makubwa kwake atakapokuwa anawasili Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam Ijumaa.

Baada ya hapo, Rage ataitisha Mkutano Mkuu wa dharula Jumapili na siku hiyo atawasimamisha Wajumbe wote wa Kamati ya Utendaji.

Rage ambaye kwa sasa yuko nchini Sudan kwa shughuli zake za kisiasa.

Hatua hiyo inafuatia kikao cha Kamati ya Utendaji ya Simba kilichokutana juzi mjini Dar es Salaam na kufikia uamuzi wa kumsimamisha Rage ambaye pia ni Mbunge wa Tabora Mjini kwa tiketi ya CCM, kwa kutokuwa na imani naye.
Rage anatuhumiwa kuchukua maamuzi mazito ya klabu bila kuwashirikisha wenzake na mengi yamekuwa yakiiweka klabu matatani. Pia, anatuhumiwa kwa ubadhirifu wa fedha za klabu na kukwamisha mambo mengi ya kimaendeleo ndani ya klabu, ikiwemo mabadiliko ya Katiba.

Baada ya kumsimamisha Rage, Kamati ya Utendaji pia ilimteua Joseph Itang’are ‘Kinesi’ kukaimu Uenyekiti wa klabu hadi hapo Mkutano Mkuu utakapofanyika.
Kinesi pia alikuwa anakaimu nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa klabu, iliyoachwa wazi na Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ aliyejiuzulu mapema mwaka huu, ambaye sasa ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Pamoja na kumsimamisha Rage, Kamati ya Utendaji pia imewasimamisha makocha wa kikosi cha kwanza, Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibaden’ na Msaidizi wake, Jamhuri Mussa Kihwelo ‘Julio’.  
Kamati imeamua kwa sasa timu itakuwa chini ya kocha wa timu ya vijana, Simba B, Suleiman Abdallah Matola ‘Veron’ ambaye atakuwa pia Msaidizi wa kocha Mkuu mpya wa kigeni, atakayetambulishwa Desemba 1, mwaka huu.

No comments:

Post a Comment