HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 20 November 2013

PATA HABARI NA RATIBA YA LIGI ZA MAJUU




DABI YA MERSEYSIDE: AGGER WA LIVERPOOL AKIRI EVERTON NGUMU!
BEKI wa Liverpool Daniel Agger anatarajia Dabi ya Merseyside, ile Mechi kati ya Klabu za Jiji la Liverpool Everton na Liverpool, Wikiendi hii itakuwa ngumu mno kama ilivyo kawaida.
Jumamosi, Uwanjani Goodison Park, Everton itaikaribisha Liverpool katika Mechi ya kwanza kabisa ya Ligi Kuu England Wikiendi hii ambayo inarejea kilingeni baada ya Wiki mbili kupisha Mechi za Kimataifa.
++++++++++++++++++++
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA:
Jumamosi 23 Novemba
[Saa za Bongo]
1545 Everton v Liverpool
1800 Arsenal v Southampton
1800 Fulham v Swansea City
1800 Hull City v Crystal Palace
1800 Newcastle United v Norwich City
1800 Stoke City v Sunderland
2030 West Ham United v Chelsea
++++++++++++++++++++
Agger amekiri kuwa Msimu huu Everton, chini ya Meneja mpya Roberto Martinez, imekuwa kali mno.
Agger amesema: “Ni juu ya Pointi 3 tu na tunatumaini tutazipata. Siku zote Dabi hii ni ngumu mno. Everton Msimu huu wameanza vizuri, wana Meneja mpya na staili tofauti kidogo.”
Pia Agger alifafanua kuwa licha ya Liverpool kuwa Nafasi ya Pili ni mapema mno kusema nani atashinda mbio za Ubingwa.
Liverpool wako Pointi 2 nyuma ya Vinara Arsenal na Everton wako Nafasi ya 6 wakiwa Pointi 3 nyuma ya Liverpool.
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA:
[Saa za Bongo]
Jumapili 24 Novemba
1630 Manchester City v Tottenham Hotspur
1900 Cardiff City v Manchester United
Jumatatu 25 Novemba
2300 West Bromwich Albion v Aston Villa
LIGI KUU ENGLAND
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
GD
PTS
1
Arsenal
11
12
25
2
Liverpool
11
11
23
3
Southampton
11
10
22
4
Chelsea
11
8
21
5
Man Utd
11
5
20
6
Everton
11
4
20
7
Tottenham
11
3
20
8
Man City
11
16
19
9
Newcastle
11
-1
17
10
West Brom
11
0
14
11
Aston Villa
11
-1
14
12
Hull
11
-5
14
13
Swansea
11
0
12
14
Cardiff
11
-6
12
15
Norwich
11
-12
11
16
West Ham
11
-2
10
17
Stoke
11
-4
10
18
Fulham
11
-9
10
19
Sunderland
11
-14
7
20
Crystal Palace
11
-15
4

BARCELONA YATHIBITISHA VALDES NJE HADI 2014
KIPA wa Barcelona, Victor Valdez, anakabiliwa na muda mrefu nje ya Uwanja baada kuumia kwenye Mechi ya Timu ya Taifa ya Spain Jumanne walipofungwa 1-0 na Afrika Kusini.
Katika Mechi hiyo iliyochezwa Nchini Afrika Kusini, Valdez, mwenye Miaka 31, alimbadili Iker Casillas wa Real Madrid wakati wa Haftaimu lakini yeye alidumu Dakika 25 tu baada kuumia na nafasi yake kuchukuliwa na Kipa wa Liverpool, Pepe Reina, ambae yuko Napoli kwa Mkopo.
Madaktari wa Timu ya Spain walisema Kipa huyo amechanika Musuli ya nyuma ya Mguu na atakuwa nje kwa Wiki 4 lakini baada ya uchunguzi wa kina hii leo imethibitika kuwa atakuwa nje kwa muda mrefu zaidi.
Hali hiyo imethibitishwa hii leo na Taarifa rasmi ya Klabu ya Barcelona kwenye Tovuti yao ambayo imesema atakuwa nje kwa muda usiopungua Wiki 6.
Pigo hili linafuatia lile la Klabu hiyo kumkosa Nyota wao mkubwa Lionel Messi ambae nae ni majeruhi na atakuwa nje kwa Wiki 6 hadi 8.
Valdez, ambae Msimu huu ameshaidakia Barca Mechi 19, atazikosa Mechi za Timu yake za UEFA CHAMPIONZ LIGI za Kundi lao dhidi ya Ajax na Celtic na Mechi za La Liga na Granada, Athletic Bilbao na Villarreal.
Kuumia kwa Valdez ambae Mkataba wake unamalizika Mwezi Juni na mwenyewe alishasema anaondoka kutaifanya Barca kusaka Kipa wa kudumu haraka.
LA LIGA
RATIBA
[Saa za Bongo]
Ijumaa Novemba 22
2300  Real Valladolid v Osasuna
Jumamosi Novemba 23
1800  FC Barcelona v Granada CF
2000  Real Sociedad v Celta de Vigo
2200  UD Almeria v Real Madrid CF
0000  Atletico de Madrid v Getafe CF
Jumapili Novemba 24
1400  Levante v Villarreal CF
1900  Rayo Vallecano v RCD Espanyol
2100  Elche CF v Valencia
2300  Sevilla FC v Real Betis
0000 Malaga CF v Athletic de Bilbao

No comments:

Post a Comment