HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 20 November 2013

BALLON D'OR: FIFA YAONGEZA MUDA UPIGAJI KURA KUSUBIRI KURA ZA RONALDO!


Ronaldo

FIFA imeongeza muda wa upigaji Kura kwa ajili ya kuchagua Mchezaji Bora Duniani kwa Mwaka 2013 ambae atashinda Tuzo ya Ballon d'Or na hali hii, Wachunguzi wamesema, itaongeza nafasi ya Cristiano Ronaldo kutwaa Tuzo hiyo baada kuonyesha uhodari mkubwa ulioifanya Nchi yake Portugal ifuzu kucheza Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwakani.

Upigaji Kura sasa utakuwa wazi hadi Ijumaa Novemba 29 wakati ulitakiwa kufungwa Novemba 15 na uongezwaji huu umedaiwa na FIFA kuwa ni kwa sababu Wapigaji Kura wengi walishindwa kuwasilisha Kura zao kwa wakati.
Ronaldo, ambae alitwaa Tuzo ya hii Mwaka 2008, Jummane Usiku alipiga Bao zote 3 wakati Portugal inaifunga Sweden 3-2 huko Stockholm na kutua Brazil kwenye Kombe la Dunia.

Lionel Messi ametwaa Tuzo hii kwa Miaka minne iliyopita.
Mshindi wa Ballon d'Or anachaguliwa kwa Kura toka kwa Makocha wa Timu za Taifa na Manahodha wao pamoja na Mwanahabari mmoja kutoka kila Nchi Wanachama wa FIFA ambapo kuna Wanachama 209.
Awali Dirisha la Upigaji Kura lilikuwa ni kati ya Oktoba 28 hadi Novemba 15.
Washindi watatajwa Januari 13 Mjini Zurich.

WAGOMBEA- Ballon d'Or: Gareth Bale (Real Madrid), Edinson Cavani (Paris St-Germain), Radamel Falcao (Monaco), Eden Hazard (Chelsea), Zlatan Ibrahimovic (Paris St-Germain), Andres Iniesta (Barcelona), Philipp Lahm (Bayern Munich), Robert Lewandowski (Borussia Dortmund), Lionel Messi (Barcelona), Thomas Muller (Bayern Munich), Manuel Neuer (Bayern Munich), Neymar (Barcelona), Mesut Ozil (Arsenal), Andrea Pirlo (Juventus), Franck Ribery (Bayern Munich), Arjen Robben (Bayern Munich), Cristiano Ronaldo (Real Madrid), Bastian Schweinsteiger (Bayern Munich), Luis Suarez (Liverpool), Thiago Silva (Paris St-Germain), Yaya Toure (Manchester City), Robin Van Persie (Manchester United), Xavi (Barcelona).

WAGOMBEA- Kocha Bora: Carlo Ancelotti (Real Madrid CF), Rafael Benítez (Napoli), Antonio Conte (Juventus), Vicente Del Bosque (Spain), Sir Alex Ferguson (Manchester United's former coach), Jupp Heynckes (Bayern Munich's former coach), Jurgen Klopp (Borussia Dortmund), Jose Mourinho (Chelsea), Luiz Felipe Scolari (Brazil), Arsene Wenger (Arsenal).

No comments:

Post a Comment