HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 18 November 2013

MAJAMBAZI YENYE SILAHA YAPORA KANGE NA KUTOKOMEA KUSIKOJULIKANA




Na Godwin Lyakurwa
TANGA
Jeshi la Polisi Mkoani  Tanga linawatafuta watu wanne kwa tuhuma za kuhusika na tukio la ujambazi wa kutumia silaha katika eneo la Kange Kata ya Maweni jjini Tanga.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Costantin Massawe(picha na Maktaba)
 
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Afisa Upelelezi Mkoa wa Tanga Aziz Kimata ameeleza kuwa tukio hilo lilitokea mnamo siku ya Jumapili Nov 16/ 2013 mnamo majira  ya saa 5:15 Usiku ambapo majambazi hao wanne mmoja akiwa na bastola walivamia baa maarufu iliyoko maeneo hayo iitwayo Bongo Pub na kupora Sh 550000/=,Tv ndogo na Vinywaji vyote mali ya mmiliki wa Baa hiyo na kisha kutoweka kusiko julikana.

Hata hivyo hakuna aliye jeruhiwa katika tukio hilo ambapo majambazi hao walifyatua risasi  hewani ili kuwatishia wananchi waliokuwa jirani na eneo hilo.

Aidha Eng Kimati ambaye ni Afisa Upelelezi Mkoa ametoa wito kwa wakaazi wa mkoa wa Tanga na vitongoji vyake kutoa taarifa za uhalifu mapema hasa kabla haujatokea iwapo watahisi mienendo isiyo salama kwa baadhi ya watu ili kuweza kudhibiti uhalifu hasa katika kipindi hiki cha mwishi wa Mwaka.
Afisa huyo ameeleza kuwa hakuna aliekamatwa  kuhusiana na tukio hilo la Ujambazi na Upelelezi ili kuwabaini watu hao unaendelea.

No comments:

Post a Comment