HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 18 November 2013

MKUU WA WILAYA YA KILINDI MKOANI TANGA AKATAA KUPOKEA RUSHWA YA SH 1100000 “WAHUSIKA WANASWA NA TAKUKURU MKOA”




TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa mkoa wa Tanga (Takukuru) imewafikisha mahakama ya wilaya ya Handeni wakazi wawili wa wilaya ya Kilindi kwa tuhuma za kutaka kutoa rushwa ya sh.1,100,000kwa mkuu wa wilaya ya Kilindi Suleima Liwowa ili atamke eneo la Elerai liwe kijiji halali na kimeundwa baada ya kupitia taratibu zote za kisheria jambo ambalo halikuwa la kweli.

Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Tanga,Edson Makala alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea Novemba 12 mwaka huu mara baada ya taasisi hiyo kuweka mtego ambao uliwekwa na ofisi ya mkuu huyo wa wilaya na kufanikiwa kuwakamata wahusika hao.

Makala alisema watuhumiwa hao  walitenda kosa la kujihusisha na vitendo vya kushawishi na kutoa hongo ya kiasi cha sh.milioni moja na laki moja kwa mkuu wa wilaya hiyo ili kulifanya jambo la eneo hilo lifanikiwe kitendo ambacho ni kinyume cha sheria.

Kamanda Makalo aliwataja washtakiwa hao kuwa ni Sharrif Lemanda Lemteka mkazi wa Lesoit Kiteto na Emanuel Ole Kileli mkazi wa Elerai kata ya Kibirashi  wilayani Kilindi na kufunguliwa kesi  ya jinai Na CC 228/2013 ambapo washtakiwa wanadaiwa kujihusisha na vitendo vya rushwa kinyume na kifungu  cha 15(b) cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa Na 11/2007.

Alisema washtakiwa wote wawili walisomewa mashtaka na mwendesha mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa George Magoti mbele ya hakimu wa wilaya ya Handeni Patrick Maligana ambapo washtakiwa wote wawili walipata dhamana baada ya kutimiza masharti yaliyotolewa na mahakama wakati kesi hiyo ikipangwa kutajwa tena mahakamani hapo Novemba 28 mwaka huu.

Aliongeza kwa kutoa wito kwa wananchi kuzingatia maadili na kutojikujihusisha na vitendo vya rushwa kwani kufanya hivyo watakuwa wameingia matatani.

No comments:

Post a Comment