![]() |
| Awadh Juma Issa (Kushoto)Ally Baru ally(kulia) wakiwa na Rage (Katikati)Picha na Bin Zubeiry |
Wekundu wa Msimbazi "SIMBA SC" imesajili wachezaji wawili kwa mpigo leo
hii, kiungo mchezeshaji Awadh Juma Issa kutoka Mtibwa Sugar ya Morogoro na Ally
Badru Ally kutoka Canal Suez ya Ligi Kuu ya nchini Misri.
Wachezaji hao wawili wa timu ya soka ya taifa ya Zanzibar wamesaini adhuhuri ya leo, nyumbani kwa Mwenyekiti wa Simba SC, Alhaj Ismail Aden Rage, Mtaa wa Samora, jijini Dar es Salaam.
Wachezaji hao wawili wa timu ya soka ya taifa ya Zanzibar wamesaini adhuhuri ya leo, nyumbani kwa Mwenyekiti wa Simba SC, Alhaj Ismail Aden Rage, Mtaa wa Samora, jijini Dar es Salaam.
Wachezaji hao walitua kwa ndege maalum na mchana
wakaenda kusaini mikataba ya miaka miwili kila mmoja na baada ya hapo,
wakarejea kwenye kambi ya Zanzibar Heroes inayojiandaa na michuano ya CECAFA
Challenge.
Akizungumza baada ya kuwasajili wachezaji hao, Rage alisema kwamba usajili huo umetokana na mapendekezo ya benchi la Ufundi la Simba SC.
“Ni wachezaji wazuri, ambao tunawajua vizuri na tumekuwa tukiwafuatilia kwa muda mrefu na tuna imani nao sana kwamba watakuja kuisaidia timu yetu,”alisema Rage.
Kwa upande wake, Ally Badru alisema kwamba
amefurahi sana kusaini Simba SC na anaamini nyota yake itang’ara huko. “Simba
SC ni timu kubwa, maarufu, naamini kabisa hapa nitafanya vizuri, kikubwa tu
naomba sapoti ya mashabiki wote,”alisema.
Kuhusu klabu yake ya Misri aliyoichezea tangu mwaka 2010, Badru alisema kwamba imemruhusu kuondoka ingawa alikuwa ana miaka miwili zaidi katika Mkataba wake na klabu hiyo.
Juma ambaye ameichezea Mtibwa Sugar kwa miaka miwili tangu alipojiunga nayo akitokea Taasisi ya Soka Tanzania (TSA) ambako alikuwa pamoja na Thomas Ulimwengu alisema kwamba amefurahi kutua Msimbazi.
“Nimefurahi sana kuja Simba SC, ni ndoto zangu za muda mrefu na sasa ni wakati wa kufanya kazi tu,”alisema.
Kuhusu klabu yake ya Misri aliyoichezea tangu mwaka 2010, Badru alisema kwamba imemruhusu kuondoka ingawa alikuwa ana miaka miwili zaidi katika Mkataba wake na klabu hiyo.
Juma ambaye ameichezea Mtibwa Sugar kwa miaka miwili tangu alipojiunga nayo akitokea Taasisi ya Soka Tanzania (TSA) ambako alikuwa pamoja na Thomas Ulimwengu alisema kwamba amefurahi kutua Msimbazi.
“Nimefurahi sana kuja Simba SC, ni ndoto zangu za muda mrefu na sasa ni wakati wa kufanya kazi tu,”alisema.

No comments:
Post a Comment