HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Sunday, 27 October 2013

UBAGUZI KWENYE SOKA



BLATTER DHIDI YA UBAGUZI


RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Sepp Blatter anataka adhabu kali zaidi ili kupambana na ubaguzi katika soka ikiwemo adhabu ya kuondoa timu mashindanoni au kuwakata alama (POINT). 
Kauli ya Blatter imekuja kufuatia Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA kuanza uchunguzi dhidi ya klabu ya CSKA Moscow baada kiungo wa Manchester City Yaya Toure kulalamika kufanyiwa vitendo vya kibaguzi na mashabiki. 
Blatter amesema faini inayotozwa na timu kucheza bila mashabiki inaonekana ni adhabu isiyotosheleza kwasasa. Rais huyo aliendelea kudai kuwa kama kweli wanataka kutokomeza suala hilo michezoni basi inapaswa adhabu kali zaidi kama kuondoa timu katika mashindano husika au kuzikata alama ziongezwe kwenye sheria ili kudhibiti mashabiki wasio na adabu.

No comments:

Post a Comment