MGOMO WA VILABU KUFANYIKA UFARANSA
VILABU
vya soka nchini Ufaransa vitafanya mgomo mwezi ujao kwa mara ya kwanza katika
miaka 40 kulalamikia mipango ya serikali kuwatoza kodi ya asilimia 75 wanaopata
mapato makubwa.
Mgomo
huo wa kwanza katika soka la Ufaransa tangu mwaka wa 1972 unatarajiwa
kuandaliwa katika wikiendi ya mwisho ya Novemba baada ya vilabu hivyo kupiga
kura kwa kauli moja dhidi ya mpango huo wenye utata wa Rais wa Ufaransa
Francois Hollande wa kutoza kiwango kikubwa cha kodi.
Rais
wa chama cha vilabu vya soka vya Ufaransa – UCPF Jean-Pierre Louvel amesema
hakutakuwa na mechi yoyote ya ligi Novemba 29 na Desemba 2. Chini ya
mapendekezo hayo, makampuni badala ya wachezaji yatahitajika kulipa kiwango cha
juu cha kodi kwa niaba ya wafanyakazi wao ambao ni wachezaji ambacho kinazidi
euro milioni moja.

No comments:
Post a Comment