EL SHAARAWY
MSHAMBULIAJI
nyota wa klabu ya AC Milan, Stephen El Shaarawy amedai kutaka kuondoka katika
klabu hiyo kwenda kusaka maisha mapya katika timu nyingine ili aweze kupata
nafasi ya kucheza.
Uamuzi wa
kinda huyo mwenye miaka 20 unazifanya klabu za Chelsea, Tottenham Hotspurs na
Arsenal kuingia vitani lakini Liverpool inaelezwa ndio wana nafasi kubwa zaidi
ya kumnyakuwa nyota huyo.
El Shaarawy
ambaye alifunga mabao 16 msimu uliopita lakini sasa amekuwa akipata wakati
mgumu kupata namba katika kikosi cha kwanza toka Mario Balotelli atue San Siro.
Wamiliki wa Liverpool wanapanga mipango ya kununua wachezaji wadogo na El
Shaarawy anaonekana kuwemo kwenye mipango hiyo.

No comments:
Post a Comment