HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Saturday, 26 October 2013



KENYA YAITEGA UN 
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta
 
Kenya imewasilisha rasmi barua kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuahirisha kesi zinazoendelea katika mahakama ya ICC dhidi ya rais Uhuru Kenyatta na naibu rais William Ruto. Pia, nchi 49 za Umoja wa Afrika zimetia saini barua iliyowasilishwa Jumanne kwa baraza hilo ikiunga mkono  kuahirishwa kwa kesi hizo dhidi ya viongozi wa Kenya.

Akizungumza na idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika Jumatano, balozi wa Kenya katika Umoja wa Mataifa  bw. Macharia Kamau alisema Kenya na Umoja wa Afrika wanasubiri kwa hamu maamuzi ya Baraza hilo.

Katika ombi lake Kenya inalitaka Baraza hilo kufikia maamuzi ya haraka  kuwawezesha viongozi wake kutohudhuria vikao vya kesi dhidi yao katika mahakama ya The Hague kwa mwaka mmoja.

Balozi Kamau alisema Kenya inakabiliwa na tishio kuu la ugaidi na ukosefu wa usalama hata  kutoka pembe ya Afrika. Alisema ombi la Kenya la  mwaka wa 2011 katika Baraza hilo halikupata majibu yaliyotegemewa na kwamba viongozi wake bw. Kenyatta na naibu rais Ruto wanahitaji kuwa nchini kusimamia shughuli za usalama na majukumu yao kama wanavyotakiwa na katiba ya nchi hiyo.

 Viongozi hao wa Kenya wanakabiliwa na mashtaka mbele ya mahakama ya kimataifa ya ICC kwa tuhuma kwamba walichochea ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2007 na mapema mwaka wa 2008.


No comments:

Post a Comment