HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Saturday, 26 October 2013



 


 Dr Slaa 
 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) hakijawasilisha taarifa zake za mapato na matumizi inayoonesha ilivyotumia fedha za ruzuku inayopewa na serikali kwa ajili ya kufanyiwa ukaguzi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kama kilivyokuwa kimedai
.
Katika taarifa yake Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi aliyotoa jana kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), vyama vilivyowasilisha taarifa za hesabu zake kwa Msajili ni vinne.

Vyama hivyo ni Chama cha Wananchi (CUF), Chama Cha Mapinduzi(CCM), Chama cha Tanzania Labour (TLP) na NCCR-Mageuzi.

Awali katika taarifa yake Chadema ilidai kuwasilisha taarifa zake za fedha kwa Msajili wa Vyama vya Siasa na zilizokaguliwa kwa mwaka wa fedha 2010/11 na 2011/12.
Chama hicho kilisema kina uthibitisho na barua ya Msajili wa vyama yenye kumb. Na CDA.112/123/01a/37 ya Septemba 4, 2012, iliyopelekwa kwa makatibu wakuu wa vyama vyote vya siasa.

Uthibitisho huo ulitolewa kukanusha taarifa ya Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe, iliyosema kuwa vyama vya siasa vinavyopata ruzuku kutoka serikalini havijawasilisha taarifa yake ya mapato na matumizi kwa ajili ya kufanyiwa ukaguzi na CAG, kwa kipindi cha miaka minne mfululizo.

No comments:

Post a Comment