HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday 7 May 2018

SERIKALI HAIJAZUIA HARAKATI ZA KISIASA: NAIBU WAZIRI MAVUNDE.

Serikali kupitia Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde,imesema kwamba haijaweka zuio kwa vyama vya siasa kufanya siasa, bali kuna sheria ambazo zinapelekea kutokea kwa hali hiyo.

Akijibu swali Bungeni kwa niaba ya Waziri Mkuu, Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde, amesema seikali haijuzia vyama vya siasa kufanya siasa, kwani imevipa uhuru vyama hivyo kufanya shughuli zake za kisiasa, isipokuwa kuna sheria za jeshi la polisi ndizo zinatoa muongozo juu ya ufanyikaji wa mikutano ya siasa na maandamano.

“"Si kweli kwamba serikali inazuia harakati za kisiasa, sheria imetoa uhuru kwa vyama kutafuta wanachama na kufanya mikutano lakini iko subject na sheria nyinginezo, ikiwemo sheria ya Police force na auxiliary service act ambayo pia imeweka masharti katika section namba 44 na 45 ya namna vyama vya siasa vinaweza vikafanya kazi zao hasa katika mikutano na maandamano mbali mbali”, amesema Anthony Mavunde.

Swali lililojibiwa lililoulizwa na Mbunge wa Rombo Joseph Selasini ambalo lilitaka serikali kusimamia sheria ikiwemo inayowaruhusu wanasiasa kufanya siasa.

No comments:

Post a Comment