HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 9 January 2018

KALI YA MWAKA... WALIOATHIRIWA NA MKOROGO KUKOSA AJIRA NCHINI GHANA.



Kitengo cha uhamiaji nchini Ghana kimewaondolea vigezo waliotuma maombi ya kazi wakati wa zoezi la kukusanya wafanyikazi wapya kwa sababu ya kubadilisha rangi ya miili yao ama maarufu kujichubua na wenye michirizi mwilini.

Msemaji wa kitengo hicho ameiambia BBC kuwa wamewaondolea vigezo kwa sababu wanaweza kupata majeraha na kutokwa na damu wakati wa mafunzo.

Baadhi ya Waghana wamepinga hatua hiyo na kuiita ya kibaguzi huku baadhi wakikasirishwa zaidi na waliondolewa vigezo kwa sababu ya kuwa na michirizi mwilini.Nao baadhi wamesifia hatua ya kuwaondelea vigezo waliobadili rangi zao za mwili.

Walioondolewa vigezo, wengine ni wenye michoro mwilini (tattoo) na wenye rasta.Wanaotuma maombi ya kutaka ajira wanapitia vipimo vya mwili na afya kama sehemu ya zoezi la kuwachuja wenye vigezo.

Watu 84,000 walituma maombi ya kazi hiyo, huku wanaohitajika wakiwa ni 500 pekee.

Mbunge mmoja, Richard Quashigah, amesema kuwa waombaji waliokataliwa wanaweza kuwapeleka waajiri hao mahakamani.
 

No comments:

Post a Comment