HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Sunday, 31 December 2017

SERIKALI YATANGAZA KIAMA KWA WAKANDARASI WASIO WAAMINIFU.



Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso amesema wizara yake haitasita kumchukulia hatua mkandarasi yeyote  atabainika kuwa chanzo chakukwamisha utekelezaji wa miradi ya maji katika maeneo mbalimbali nchini.

Naibu Waziri huyo ameyasema hayo wakati akikagua mradi wa maji wilayani Momba  Mkoani Songwe.

"Serikali inataka mradi huu  na miradi mingine yote ya maji nchini ikamilike kwa wakati na wananchi waanze kufaidi matunda ya Serikali yao, ndio maana nipohapa kufuatilia hilo na wakandarasi waliopewa kazi wahakikishe wanafanya kazi usiku na mchana ili kufanikisha hilo la si hivyo serikali haitasita kuwachukulia hatua.,’’ amesema Mh. Aweso.

Naibu Waziri huyo yupo Mkoani Songwe katika ziara yake ya kikazi ya kukagua miradi mbalimbali.

No comments:

Post a Comment