HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Saturday, 23 December 2017

MCHAKATO WA MABADILIKO YANGA WAIVA, WATAKAOONGOZA SAFARI WAPATIKANA.


Kamati ya utendaji ya Yanga Ijumaa Desemba 22, 2017, imetangaza majina ya wajumbe sita iliyowateua kusimamia mchakato wa mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji.

Kaimu mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga amesema kamati hiyo ambayo tayari imeshaanza mchakato huo, itaongozwa na Mwenyekiti, Wakili Alex Mgongolwa ambaye pia ni mwanasheria wa klabu hiyo.

Wajumbe wengine watano wa kamati hiyo ni aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick, Profesa Mgongo Fimbo ambaye ni mtaalamu wa masuala ya katiba na sheria za ardhi na George Fumbuka , mtaalamu wa masuala ya uwekezaji.

Wajumbe wengine wa kamati hiyo ni Felix Mrema ambaye pia ni mtaalamu wa masuala ya fedha na uchumi sambama na Mwenyekiti wa kamati ya fedha na mipango wa Yanga, Mohammed Nyengi "Sisi kama uongozi tuna imani kamati hii itafanya kazi kwa ufanisi wa hali ya juu kwa sababu inaundwa na wajumbe wenye utaalamu wa hali ya juu ya masuala ya uwekezaji na pia wana mapenzi na klabu yetu," alisema Sanga.
Miaka 10 iliyopita Yanga ilianza mchakato wa uuzwajiwa wa hisa zake kwa muhtasari huu unaainisha ufafanuzi wa kazi na mapendekezo ya kamati maalumu iliyopitia rasmu ya uuzaji wa hisa kwa kampuni ya Advertisement (Public Company) kulingana na muafaka uliofikiwa na wanayanga mnamo 22/6/2006.

Katika muafaka huu wana –yanga walikubaliana kuwa kitu kimoja na kwamba kuwepo Kwa klabu na Kampuni ya umma (Public Company) ambayo wanachama watakuwa na Hisa na sauti, tofauti na muundo wa kampuni ya hapo awali ambayo ilikuwa ya binafsi (Private Company).

Katika kufanikisha masuala ya uanzishwaji wa kampuni ya umma (Public Company) na masuala yote ya hisa watu watatu kutoka kila kundi (miongoni mwa makundi matatu yaliyokuwepo kabla ya kufikia muafaka ambayo ni yanga kampuni , yanga asili na yanga academia) waliteuliwa kama wawakilishi wa makundi wa makundi yao.

Kazi ya kamati hii maalumu ya watu watatu zilikuwa mbili, kwanza kuandaa rasimu ya kampuni ya umma na pili kuandaa mchanganuo mzima wa utekelezaji wa muafaka kwa vitendo ambayo itawasilishwa kwa wanachama na yalihitaji muda wa kutosha kuyapitia.

Kifungu kwa kifungu ili kuhakikisha kwamba inakidhi matakwa ya kampuni ya umma (Public Company) kama unavyoagiza muafaka na kukidhi matakwa ya kisheria.

Hata hivyo; mpango huo ulishindikana hadi mwaka huu ambako umeanza tena na sasa imeundwa kamati nyingine ya watu saba.

No comments:

Post a Comment