HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 24 October 2016

KUMEKUCHA JANGWANI, KOCHA MPYA YANGA ATUA DAR...PLUJM MWAMBUSI BAIBAI...



MABADILIKO ya benchi la Ufundi la Yanga SC yameiva kufuatia kuwasili kwa kocha Mzambia, George Lwandamina jana tayari kusaini Mkataba.
Mzambia, George Lwandamina
Kocha Mkuu, Hans van der Pluijm raia wa Uholanzi na Wasaidizi wake, Juma Mwambusi, kocha wa makipa Juma Pondamali na Meneja Hafidh Saleh wote wazalendo wataondoka.

Na Mzambia, George Lwandamina atakuwa Kocha Mkuu, akisaidiwa na wazalendo Charles Boniface Mkwasa, Manyika Peter kocha wa makipa na Meneja, Sekilojo Chambua.  

Pluijm amejikuta katika wakati mgumu baada ya Yanga kuambulia pointi 21 kati ya 30 za mechi 10 za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Yanga SC imetoa sare tatu, imefungwa mechi moja na kushinda sita tangu kuanza kwa Ligi Kuu – hiyo ikiwa ni mbali na kupoteza mchezo wa Ngao ya Jamii mbele ya Azam kwa penalti 4-1 baada ya sare ya 2-2.

Na baada ya mchezo wa Oktoba 1, wakilazimishwa sare ya 1-1 na mahasimu, Simba SC waliokuwa pungufu kwa sehemu kubwa kufuatia Nahodha wao, Jonas Mkude kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 29, baadhi ya viongozi wa Yanga wamependekeza mwalimu huyo aondolewe.

Lakini habari zinasema Pluijm atakuwa Mkurugenzi wa Ufundi katika mabadiliko haya.

No comments:

Post a Comment