HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 24 June 2016

TAARIFA MPYA ZA USAJILI JUNI-2016, LIVER, CHELSEA, MAN CITY,MADRID VITANI KUSAJILI.



CLOPP AONGOZA MBIO ZA KUMSAINI SADIO MANE
Meneja wa klabu ya Liverpool, Jurgen Klopp huenda akaizidi keta klabu ya Man Utd katika mpango wa usajili wa mshambuliaji kutoka nchini Senegal pamoja na klabu ya Southampton, Sadio Mane.Klopp ameonyesha dhamira hiyo, kufuatia kuafiki mpango wa usajili wa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 24, ambao huenda ukamgharimu kiasi cha Pauni milioni 25.

Meneja huyo kutoka nchini Ujerumani, ameonyesha kuwa na dhamira ya kweli katika mpango huo, tofauti na ilivyo kwa Man Utd ambao mara kadhaa hawajihusishi sana na harakati za usajili wa Mane.
Endapo Mane, ataondoka Southampton, wakati wa majira ya kiangazi kwa ada ya uhamisho wa Pauni milioni 25, ataiwezesha klabu hiyo kujipatia faida ya Pauni milioni 13.

Miaka miwiwli iliyopita, The Saint walimsajili mshambuliaji huyo kwa ada ya uhamisho wa Pauni milioni 12, akitokea nchini Uswiz alipokua akiitumikia klabu ya Salzburg.

Klopp alianza kuvutiwa na Mane, tangu alipoonyesha kiwango cha hali ya juu wakati wa mchezo wa ligi kuu ya soka nchini England msimu uliopita, kati ya Southampton dhidi ya Liverpool, ambao ulimalizika kwa majogoo wa jiji kukubali kisago cha mabao matatu kwa mawili.

CHELSEA YAPANIA KUNASA SAINI YA BEKI YA NAPOLI
KLABU ya Chelsea inadaiwa kuanza kumuwania beki wa Napoli Kalidou Koulibaly kwa kutoa ofa ya paundi milioni 19.2. Chelsea wamekuwa wakimhusudu kwa kiasi kikubwa beki huyo wa kimataifa wa Senegal, ambaye ameingia katika mzozo na klabu yake kuhusiana na uhamisho wake.

Hata hivyo, ofa hiyo ya Chelsea tayari imeshakataliwa na Napoli wamedai wanataka kitita cha paundi milioni 30 ili waweze kumuachia nyota huyo mwenye umri wa miaka 24. Napoli walichukizwa na Koulibaly kufuatia madai aliyotoa kuwa yuko tayari kuzungumza na Chelsea.

Beki huyo amesema hajazungumza na Antonio Conte lakini anadhani hilo litafanyika hivi karibuni. 

NOLITO ANUKIA MAN CITY
KLABU ya Manchester City, inadaiwa kukaribia kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Hispania, Nolito kutoka Celta Vigo. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 29 amethaminishwa kwa kiasi cha euro milioni 18 katika mkataba wake, na rais wa Celta Vigo Carlos Mourino tayari ameshadokeza kuwa anategemea ataondoka kiangazi hiki.

Taarifa zilizotolewa na gazeti la Gurdian la Uingereza zimedai kuwa City wana uhakika wa kukamilisha dili hilo na kuongeza kuwa Nolito tayari ameshakubali mambo binafsi katika mkataba wa miaka mitatu atakaopewa wenye thamani ya euro milioni nne kila msimu. Mchezaji huyo wa zamani wa Barcelona, ambaye amecheza katika mechi zote tatu za Hispania katika michuano ya Ulaya inayoendelea nchini Ufaransa, amekuwa pia akihusishwa na tetesi za kurejea Camp Nou.

Nolito ambaye atafikisha miaka 30 Octoba mwaka huu, aliondoka Barcelona na kwenda Benfica mwaka 2011 kabla ya kujiunga na Celta Vigo miaka miwili baadae.

MADRID YATHIBITISHA KUMREJESHA MORATA. 
KLABU ya Real Madrid imethibitisha kuwa Alvaro Morata atarejea Santiago Bernabeu kipindi hiki cha kiangazi. Taarifa hizo zimekuwa mapema baada ya mkurugenzi mtendaji wa Juventus Beppe Marotta kubainisha kuwa Morata anategemewa kurejea Madrid.

Madrid walikuwa na nafasi ya upendeleo ya kumnunua tena Morata mwenye umri wa miaka 23, ikiwa ni sehemu ya mkataba uliopelekea nyota huyo wa kimataifa wa Hispania kujiunga na Juventus miaka miwili iliyopita na sasa wamethibitisha kufanya hivyo.

Katika taarifa yao iliyotumwa katika mtandao, Madrid walithibitisha taarifa hiyo na kudai kuwa Morata atajiunga na mazoezi ya maandalizi ya msimu mpya wa La Liga chini ya meneja Zinedine Zidane. Hata hivyo, taarifa zinadai kuwa Madrid wanaweza kumuuza Morata kwa klabu nyingine ili wapatefaida.

No comments:

Post a Comment