HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 4 March 2016

BREAKING..NEWSS... MMILIKI WA CHELSEA AMTAJA KOCHA MPYA WA KLABU HIYO.

MMILIKI wa Klabu ya Chelsea Roman Abramovich amewaambia Wachezaji wa Klabu hiyo kuwa Antonio Conte ndie atakuwa Meneja mpya Msimu ujao kwa mujibu wa ripoti toka Italy.
Conte, mwenye Miaka 46, ni Meneja wa Timu ya Taifa ya Italy na Mkataba wake unamalizika mara baada ya kwisha kwa EURO 2016 mapema Mwezi Julai.Kabla kushika wadhifa Timu ya Taifa ya Italy, Conte alikuwa Kocha Mkuu wa Juventus kuanzia 2011 hadi 2014 na kuiwezesha kutwaa Mataji Matatu ya Ubingwa wa Italy mfululizo.

Kwa mujibu wa Jarida la Italy, Corriere dello Sport, Abramovich amewahakikishia Wachezaji wa Chelsea kuwa Conte ndie Meneja mpya wakati alipokutana na Kikosi chote kwenye Kituo cha Mazoezi cha Timu hiyo huko Cobham Mjini London.

Hivi sasa Chelsea wana Meneja wa muda Guus Hiddink ambae Mkataba wake unamalizika mwishoni mwa Msimu baada ya kuteuliwa kuchukua nafasi ya Jose Mourinho alieondolewa Mwezi Desemba.

Tangu wakati huo, Hiddink ameisimamisha wima Chelsea na kupanda kwenye Ligi Kuu England hadi Nafasi ya 10 toka Nafasi za mkiani Mwezi Desemba ikiwa sasa Pointi 8 tu nyuma ya Timu ya 4 kwenye Ligi.

No comments:

Post a Comment