HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 3 December 2015

AZAM WAELEZA SIRI YA KUWEKA KAMBI YAO TANGA.




Kocha Mkuu wa Azam FC, Stewart Hall, ameweka bayana sababu ya kuweka kambi jijini Tanga kuwa ni kutaka kujenga ‘fiziki’ na kuwaongezea kasi wachezaji wake.
Katika maandalizi hayo, Hall amesema amepanga kucheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya Mgambo na African Sports lakini akaweka sababu za kuzichagua mechi hizo badala ya Coastal kwa kusema anataka kuzisoma mapema kabla ya kukutana nazo kwenye mechi zijazo.

“Ukiangalia hatujakutana na timu hizi, tuna mchezo na Mgambo hapahapa Mkwakwani kama ilivyo kwa African Sports pia hatujacheza nao, kwa hiyo niliona kuna kila sababu ya kuziona kipindi hiki kabla ya kukutana kwenye mechi zenyewe.

“Hakukuwa na sababu ya kucheza na Coastal, maana tumeshakutana na malengo yangu kwa sasa ni kwa wapinzani wangu wajao,” alisema Muingereza huyo.
Azam FC jana ilicheza mechi ya kirafiki na kutoka sare ya mabao 1-1 dhidi ya Mgambo Shooting ikiwa ni mechi yake ya kwanza baada ya kuweka kambi hiyo ya Tanga.

Wiki ijayo, Azam itakipiga na Simba katika Ligi Kuu Bara, kisha kuwafuata Majimaji mkoani Ruvuma, kabla ya kukipiga na Mgambo, Januari 20, 2016 kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

No comments:

Post a Comment