HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 30 November 2015

JOHN CENA NA COBE BRAYANT "MASTAA WANAOIKACHA MICHEZO ILIYOWATOA"



John Cena.
Nyota wa mieleka ya maonyesho ya WWE, John Cena, amedai kuachana na shoo hiyo iliyokuwa ikioneshwa kwenye televisheni na kufanya kitu kingine tofauti.

Cena, amedai kuwa amekuwa katika ulimwengu wa mieleka kwa zaidi ya miaka 13 na kusema kuwa amechoshwa na aina hiyo ya maisha.
Sambamba na hilo amedai kuwa amepata dili la shoo nyingine ya televisheni ya Fox itakayokuwa ikionyesha maisha yake halisi itakayoenda kwa jina la ‘American grit’.

Cena amesema kujitoa kwake kutafungua milango kwa wakali wapya WWE na kudai kuwa sasa anataka kuweka nguvu zake pia katika uigizaji wa filamu.

KOBE BRYANT KUSTAAFU KIKAPU MWAKANI.
MCHEZAJI nyota wa Ligi ya Mpira wa Kikapu nchini Marekani-NBA, Kobe Bryant ambaye anahesabiwa kama mmoja ya wachezaji bora kabisa katika historia, anatarajiwa kustaafu mchezo huo mwishoni mwa msimu.
Bryant amefunga vikapu 32,683 katika kipindi cha miaka 20 alichoichezea timu ya Los Angeles Lakers na kumfanya kushika nafasi ya tatu katika orodha ya wafungaji wa wakati wote wa NBA. 

Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 37 ambaye ana medali za dhahabu za mashindano ya Olimpiki, amekuwa akisumbuliwa na majeruhi katika misimu ya karibuni na kumfanya kuwa chini ya kiwango msimu huu akiwa na Lakers. 

Bryant alitajwa kama Mchezaji Mwenye Thamani Zaidi wa NBA mwaka 2008 na amewahi kuchaguliwa katika kikosi cha NBA All-Star kwa nyakati 17 tofauti. Mchezo wa mwisho wa Bryant unatarajiwa kuwa dhidi ya Utah Jazz utakaochezwa Aprili 13 mwakani.

No comments:

Post a Comment