HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Saturday, 11 April 2015

MAMBO MUHIMU USIYOYAJUA KUHUSU DABI YA JIJI LA MANCHESTER KESHO..!!!



MENEJA wa Manchester United anaetoka Uholanzi Louis Van Gaal alifungwa Dabi yake ya kwanza ya Jiji la Manchester Novemba Mwaka Jana kwa Bao la Sergio Aguero huko Etihad.
Hicho kilikuwa kipigo cha 4 mfululizo kwa Man United mikononi mwa Mahasimu wao City lakini Van Gaal ameapa safari hii hilo halitatokea Jumapili Uwanjani Old Trafford wakati City watakapotua kucheza Mechi muhimu mno ya Ligi Kuu England.

Leo Van Gaal amezungumza huko Carrington, Kituo cha Mazoezi cha Man United, na kusema: "Naiota hii Dabi, kila Mchezaji anaota ushindi!"
Licha ya kuwa ni Dabi, lakini kama Juzi alivyotamka Kepteni wa Man United, Wayne Rooney, kwamba ushindi unaleta kiburi cha majivuno lakini pia safari hii kugombea 4 Bora nako ndio kunaleta changamoto kubwa.

Hivi sasa Man United wapo Nafasi ya 3 wakiwa Pointi 1 mbele ya City na ushindi kwao utawapa pengo la Pointi 4 dhidi ya City.
Van Gaal amesema: "Unataka kushinda kwani ni hatua kubwa katika Msimamo. Ukishinda Nafasi ya 3 itapatikana na Mwezi mmoja uliopita, ukiniondoa mimi, hakuna aliedhani hili linawezekana!"

Kwa fomu ya sasa ilivyo, Man United wanaingia kwenye Dabi hii wakiwa na matumaini makubwa ya ushindi baada ya kushinda Mechi 5 mfululizo za Ligi wakati City wameshinda Mechi 2 tu kati ya 7 za Mashindano yote.
Hata hivyo, Van Gaal amesisitiza hilo halina maana kwani hii ni Dabi na Gemu spesho.
Vile vile Van Gaal ameponda pale alipokumbushwa historia ya hivi karibuni ya kufungwa mfululizo na City.

Amenena: "Hiyo si Historia yangu!"
Aliongeza: "Nisemeje? Tumefungwa 1-0. Hiyo ndio historia yangu, Gemu ya mwisho tuliyocheza nao na tulipata Kadi Nyekundu Dakika ya 39!"
Katika Mechi hiyo iliyochezwa Etihad, Chris Smalling ndie aliepewa Kadi Nyekundu baada ya Kadi za Njano mbili.

LIGI KUU ENGLAND
**Saa za Bongo
Jumamosi Aprili 11
1445 Swansea v Everton  
1700 Southampton v Hull  
1700 Sunderland v Crystal Palace  
1700 Tottenham v Aston Villa  
1700 West Brom v Leicester  
1700 West Ham v Stoke  
1930 Burnley v Arsenal

Jumapili Aprili 12
1530 QPR v Chelsea  
1800 Man United v Man City  

Jumatatu Aprili 13
2200 Liverpool v Newcastle  

No comments:

Post a Comment