HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 7 April 2015

'inasikitisha" UZEMBE WA TANESCO MUHEZA WAGHARIMU MAISHA YA MTOTO WA MIAKA 7..!



Wakazi wa kijiji cha Mtambwe Kitongoji cha Shauri Moyo Wilaya ya Muheza wamelalamikia Shirika la Ugavi la Umeme nchini Tanesco Walayani humo kwa kuunganishia umeme wakazi kiolela na kusababisha kifo.

Wakazi hao wamesema wamekuwa wakitoa taarifa kwa uongozi wa Tanesco wilayani humo baada ya kushuhudia nguzo imefungwa na inapeleka umeme katika makazi ya watu bila kukamilika kwa baadhi ya vifaa bila kushughulikiwa hadi jumamosi ya April 4 shoti ya umeme imegharimu maisha ya mtoto Aisha Kombo mwenye umri wa miaka saba. 

Nguzo iliyogharimu maisha ya mtoto Aisha

Mtoto huyo ambae ni mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Mdote alipoteza maisha wakati akicheza maeneo ya jirani na nguzo hiyo.
Akizungumzia tukio hilo baba mzazi wa mtoto Aisha, Kombo Ramadhani Kombo amesema amesikitishwa sana na uongozi wa Tanesco kutokuwa makini katika uwekaji nguzo za umeme ambazo ni hatari kwa watu walika zote.

Kombo amesema mtoto Aisha alikuwa akicheza katika eneo hilo wakati kulikuwa na manyunyu ya mvua na kugusa waya uliotoka katika nguzo na kujikuta akipoteza maisha ghafla.
Hata hivyo mwandishi wetu alifika katika eneo la tukio na kuona jinsi nguzo hiyo ilivyokosa vifaa muhimu vya kuzuia umeme usishuke ardhini kutoka juu ya nguzo. 

Mwenyekiti wa kitongoji cha shauri moyo Seffu Twenye amesema mara mbili walitoa taarifa katika ofisi ya tanesco lakini hakuna utekelezaji wowote uliofanyika hadi mtoto huyo alipokufa
Vilevile amesema sio nguzo hiyo peke yake ila anashangazwa sana jinsi ya uunganunishaji wa umeme bila kuweka vikombe na kuomba uongozi wa shilika la umeme Tanesco liwaeleze kama ni mbinu mpya ya uunganishaji wa umeme huo unaoitwa umeme wa Obama.

No comments:

Post a Comment