HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday 1 December 2014

IKUWA LEO NI SIKU YA UKIMWI DUNIANI "hizi ni Taarifa Muhimu za Ugonjwa huo Hatari"



Upungufu wa Kinga Mwilini (kwa kifupi UKIMWI; kifupi cha Kiingereza AIDS) ni ugonjwa unaotokana na virusi inayoitwa VVU na inayoshambulia mwili kwa kuondoa nguvu zake za kupambana na maradhi.
Ugonjwa huu umeua watu zaidi ya milioni 36 hasa wanaoishi Kusini mwa Afrika kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani. Kwa mwaka 2005 pekee watu milioni 3.1 wamefariki na 570,000 kati yao ni watoto.
UKIMWI hadi hivi sasa haina dawa.
Tarehe ya kwanza ya mwezi wa kumi na mbili kila mwaka ni siku ya UKIMWI duniani.
Maana ya jina
Ukosefu maana yake ni kwamba watu hawatungwi na ugonjwa huo, bali wanaupata baada ya kuambukizwa virusi ya UKIMWI.
Kinga inahusu mfumo wa kinga ambao ni sehemu ya mwili dhidi ya ugonjwa.
Mwili usio na kinga unapatwa na matatizo mbalimbali kwa sababu mfumo wa kinga umeharibika, na hauwezi kupigana na ugonjwa wowote.
Asilimia ya watu wenye umri wa miaka 15–49 walioambukizwa nchi kwa nchi (2011).
Mwaka 2012 walau watu wapatao 35,300,000 walikuwa wakiishi na VVU. Watu wengi wenye VVU hawajui kuwa nayo. Kwa sababu hiyo, idadi halisi ya watu wanaoishi na VVU haijulikani.
Wengi kati ya watu wenye VVU huishi katika Afrika. Wengi kati ya watoto ambao hufariki dunia kutokana na UKIMWI pia wanaishi barani Afrika.
Wapi VVU ilianza
Wanasayansi wengi wanaamini binadamu wa kwanza ambaye alipata VVU (kwa Kiingereza HIV) alikuwa Afrika Magharibi ya Kati. Hii ilitokea mwishoni mwa karne ya 19 au mwanzoni mwa karne ya 20, wakati virusi ya SIV kutoka kwa nyani au sokwe ilikwenda kwa binadamu.
VVU na UKIMWI
Si kila mtu ambaye ana VVU ana UKIMWI. Wakati watu wanapata VVU, wanaweza kuwa na afya kwa miaka mpaka akakutwa na aina maalumu ya magonjwa na vipimo vya damu vikionyesha kuwa ina idadi ndogo sana ya seli nyeupe za damu ambazo ndizo zinazopambana na maambukizi.

Kuna maradhi ambayo kwa kawaida ni ishara kwamba mtu ana UKIMWI kwa kuwa watu wenye afya njema hawapati magonjwa haya, kwa sababu mfumo wa kinga mwilini una nguvu ya kutosha ya kupigana na magonjwa hayo. Hivyo kupata ugonjwa wa aina hiyo ni ishara kwamba mfumo wa kinga umeharibika.
Baadhi magonjwa hayo ni:
Sarkoma ya Kaposi - aina ya kansa ambayo kwa kawaida huathiri ngozi (mara nyingi husababisha vidonda vyekundu au zambarau, au majeraha juu ya ngozi). Wakati mwingine huathiri tu ngozi, bali pia mifumo mingine katika mwili.
Retinitis - virusi zinashambulia nyuma ya jicho.
Pneumocystis carinii (kifupi PCP) - aina ya pneumonia, magonjwa ya kuambukiza ya mapafu. PCP ni maambukizi ya kawaida kwa wagonjwa wa UKIMWI.
Toxoplasmosis - ugonjwa unaosababishwa na vimelea, ambao unaweza kusababisha matatizo katika mifumo ya ubongo na mingine katika mwili.
Kansa ya kizazi - ambayo huwa inaenea.
Matibabu
Kuna dawa za kusaidia watu wenye UKIMWI. Hizi zinaitwa dawa za kurefusha maisha. Dawa za kurefusha maisha haziwezi kutibu UKIMWI. Hii ina maana kwamba haziwezi kufanya virusi zote kuondoka mwili wa mtu. Lakini zinaweza kuwasaidia watu kupambana na virusi ya UKIMWI kwa mifumo yao ya kinga kufanya kazi vizuri zaidi. Hivyo dawa za kurefusha maisha si tiba kabili kwa virusi ya UKIMWI.

Watu wenye VVU / UKIMWI ambao kuchukua dawa za kurefusha maisha wanaweza kuishi muda mrefu, bila kupata maradhi yanayothibitisha UKIMWI.
Lakini baada ya muda mrefu, virusi za HIV zisizouawa na dawa hizo hujifunza jinsi ya kupambana nazo na hivyo zinakuwa sugu kwa dawa hizo.
Wakati mwingine HIV ni sugu kwa dawa moja, lakini dawa nyingine inaweza kutumika. Ili kupunguza uwezekano wa upinzani kutokea, watu wenye UKIMWI huchukua dawa zaidi ya moja kwa wakati mmoja. Wanaweza kuchukua madawa 2-4 kwa mara moja. Hii wakati mwingine inaitwa cocktail ya UKIMWI. Lakini baada ya muda mrefu, HIV kujifunza kuwa sugu kwa dawa nyingi. Hapo hakuna zaidi ya kuwatibu. Hivyo wanasayansi kuendelea kujaribu kupata dawa mpya ya kupambana na VVU.
Dawa tano muhimu za wenye VVU ni:
D4T (stavudine)
3TC (Lamivudine)
NVP (nevirapine)
AZT (zidovudine)
EFZ (efavirenz)
Bila dawa hizo, kwa kawaida mtu mwenye VVU anaweza akaishi miaka 9-11.
Mayatima
Watu wengi ambao wanakufa kutokana na UKIMWI, hasa katika Afrika, huacha watoto ambao bado ni hai, na ambao wanaweza wanahitaji msaada na huduma.
KUMBUKA
Leo (Dec 01) ni maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu inaendelea kuwa “TANZANIA BILA MAAMBUKIZI MAPYA YA VVU; VIFO VITOKANAVYO NA UKIMWI NA UNYANYAPAA INAWEZEKANA”. Kauli mbiu hii inalenga kutoa msukumo wa utekelezaji wa mikakati ya kudhibiti UKIMWI kitaifa na kimataifa ili kufikia azma ya sifuri tatu (3) yaani maambukizi mapya sifuri, vifo sifuri na unyanyapaa sifuri ifikapo mwaka 2015. Kauli mbiu hii inahimiza utekelezaji wa dhati wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia (Millennium Development Goals-MDGs) na maazimio yaliyowekwa kwenye Mkutano Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu UKIMWI uliofanyika mwaka 2001 Jijini New York, Marekani.

No comments:

Post a Comment