HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 25 November 2014

VIJANA DUGA TANGA SASA KUJA NA VIDEO YA VIJANA NI NURU YA ULIMWENGU.

Na, DANIEL RAPHAEL, TANGA.
Kwaya ya vijana usharika wa Kana mtaa  wa Duga jijini Tanga wapo katika maandalizi yao ya mwisho ya  kujiandaa kutoa mkanda wa video wa albamu yao ijulikanayo kama vijana ni nuru ya ulimwengu.

Akizungumza na mtandao huu mwalimu wa kwaya hiyo Atanasi Jonh amesema wanajisikia furaha kufika hatua walionayo sasa na kusema kwao ni jambo la kujivunia.
Hata hivyo wanatarajia kufanya harambee kwa ajli ya kupata pesa ya kuanzisha miradi mbalimbali ambayo itawawezesha katika kuiendeleza huduma yao ya uimbaji.
“Tunamshukuru Mungu kwa kutuwezesha kufikia hatua hii tulionayo sasa kwani tulikuwa tunaisubiria kwa shauku kubwa ili kuweza kutoa video yetu” Alisema John”
Aidha amewashukuru washarika pamoja na watu mbalimbali ambao walijitoa kwa hali na mali katika kufanikisha shughuli hiyo ambapo pia amewataka wasife moyo katika kumtumikia mungu kaitika roho na kweli.
Aidha amewaasa waimbaji wengine kuboresha huduma zao ili waweze kuisambaza injili ya yesu kristo katika njia ya kweli na impasayo mungu.

No comments:

Post a Comment