HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 25 November 2014

“KIPIGO CHA MAN ARSENAL HAKUKALIKI” MATAJIRI WA ARSENAL WAMJIA JUU WENGER




MMILIKI wa Arsenal ambae ni wa Pili kwa wingi wa Hisa zake, Alisher Usmanov, amedai msimamo wa Meneja wao Arsene Wenger ndio unazuia Klabu hiyo kupanda juu na sasa inabidi Meneja huyo akiri makosa yake.

Usmanov, Raia wa Uzbekistani anaemiliki Asilimia 30 ya Hisa za Arsenal ambazo ni za pili kwa wingi wake, ameongea mara baada ya Klabu yao kuchapwa 2-1 na Manchester United hapo Jumamosi Uwanjani kwao Emirates.
Arsenal sasa wamepoteza Mechi 11 kati ya 15 walizocheza mwishoni na Man United na kushinda moja tu na Msimu huu kwenye Ligi Kuu England wameshinda Mechi 4 tu kati ya 12 walizocheza.
Usmanov ametamka: “Uwezo wa Timu upo lakini hamna mchanganuo wa kitaalam wa makosa yetu na kuyakubali. Hakuna mwerevu yeyeto anaeweza kudumu ikiwa hakubali makosa yake. Pale ukikubali makosa yako ndio unayaondoa. Nataka hili kwa Klabu yangu!”

Aliongeza: “Tunarudia yale yale Mwaka hadi Mwaka. Tuko juu kufuzu kucheza UEFA CHAMPIONZ LIGI lakini kila mara tunatolewa Raundi ya Mtoano tu. Nikiwa mwekezaji sifurahii hilo. Napenda msimamo wa Wenger. Lakini misimamo ni kizuizi. Na vizuizi Siku zote ni njia potofu. Ndio maana Makocha wasiokuwa na misimamo wanakuwa Makocha wa Timu Bora!”
Usmanov alimalizia: “Maoni yangu, tena nayaweka bayana, tunahitaji kuimarisha kila pozisheni ili tuwe sawa na Chelsea na Man City hapa England na Ulaya sawa na Real, Barcelona, Paris Saint-Germain, Bayern Munich na Klabu nyingine!”
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA:
**Saa za Bongo
Jumatatu Novemba 24
2300 Aston Villa v Southampton 
Jumamosi Novemba 29
1545 West Brom v Arsenal
1800 Burnley v Aston Villa          
1800 Liverpool v Stoke              
1800 Man Utd v Hull                 
1800 QPR v Leicester                
1800 Swansea v Crystal Palace            
1800 West Ham v Newcastle                
2030 Sunderland v Chelsea                  
Jumapili Novemba 30
1630 Southampton v Man City    
1900 Tottenham v Everton                

No comments:

Post a Comment