HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Saturday, 29 November 2014

UKWELI KUHUSU AJALI YA MKANYAGENI TANGA "13 WALIPOTEZA MAISHA"



WATU 13 wamekufa na wengine zaidi ya 19 kujeruhiwa vibaya katika ajali ya barabarani, iliyohusisha basi dogo la abiria aina ya Toyota Double Coaster, linalosafiri kati ya mjini Tanga na Lushoto, kugongana na lori la mizigo aina ya Scania, lililokuwa likitokea Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga, Juma Ndaki, ajali hiyo ilitokea juzi eneo la Mkanyageni saa moja asubuhi wakati magari hayo yalipokuwa yanapishana.

Alisema ajali hiyo, ilihusisha basi dogo lenye namba za usajili T 410 BJD lililokuwa likiendeshwa na Bakari Musa na lori lenye namba za usajili T 645 LBJ likiwa na tela lenye namba T 605 ABJ, lililokuwa likiendeshwa na Benjamin Abeid.
Alisema chanzo cha ajali hiyo ni lori hilo, lililokuwa likitokea upande wa Dar es Salaam kwenda Tanga, ambapo baada ya kufika eneo la tukio lilizidi upande wa kulia na kuligonga basi hilo la abiria na kusababisha ajali.
Akizungumzia ajali hiyo, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dk Aisha Mahita alisema maiti na majeruhi wa ajali hiyo, wamepelekwa katika Hospitali Teule ya Wilaya ya Muheza.
Dk Mahita alisema majeruhi waliopokelewa hospitalini hapo ni 25, ambapo kati yao 19 ni wanaume na 6 ni wanawake.

“Majeruhi baadhi wamepata vidonda na wengine wamevunjika mikononi na miguu, lakini wanaendelea kupatiwa matibabu hapo teule huku majeruhi wawili kati ya hao wakiwa wamelazwa kwenye chumba cha uangalizi maalum (ICU),” alisema.
Kuhusu abiria waliopoteza maisha katika ajali hiyo, Dk Mahita alisema kati yao wanaume ni saba na wanawake ni watano, ambapo tayari maiti saba wameweza kutambuliwa na ndugu zao.
Kutokana na ajali hiyo, Rais Jakaya Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dk Rajabu Rutengwe kuomboleza vifo vya abiria hao, akisema: “Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kupotea ghafla kwa maisha ya watu 13 na wengine kadhaa kujeruhiwa katika ajali ya barabarani iliyotokea katika Mkoa wako wa Tanga”.

Rais Kikwete alisema “Naomba upokee salamu zangu za rambirambi kutoka dhati ya moyo wangu kutokana na vifo hivyo, na kupitia kwako, naomba salamu za pole ziwafikie watu wote waliopotelewa na ndugu na jamaa zao kwenye ajali hiyo”.
Alisema anawaomba wote waliopoteza ndugu na jamaa zao kwenye ajali hiyo, wawe watulivu na wavumilivu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo, na aliwahakikishia kuwa yuko pamoja nao katika kipindi chote cha maombolezo.
“Kwa wote waliojeruhiwa kwenye ajali hiyo, namwomba Mungu awajalie ahueni na wapone haraka, ili warejee tena katika hali zao za kawaida. Namwomba Mola azipokee na kuzilaza mahala pema peponi Roho za Marehemu wote, Amina”, alisema Rais Kikwete.

No comments:

Post a Comment