HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 5 August 2014

MWENGE WA UHURU KUZINDUA MIRADI KUMI YA MAENDELEO KATIKA MKOA WA KASKAZINI PEMBA



Na Msanja Mbula. Pemba
Jumla ya Miradi kumi na moja yenye thamani ya  shilingi milioni 305, 650,050 /= inatarajia kufunguliwa , kuzinduliwa na kuwekewa mawe ya msingi na mwenge wa uhuru katika Mkoa wa Kaskazini Pemba .

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mhe Dadi Faki Dadi amesema kuwa miradi hiyo imeibuliwa na wananchi na imelenga katika kuwapunguzi usumbufu katika upatikanaji wa huduma za kijamii .

Mkuu huyo wa Mkoa amefafanua kwamba ukiwa katika Wilaya ya Wete , Mwenge wa uhuru utatembelea  miradi saba yenye thamani ya shilingi milioni  226,490,050 .

Aidha ameeleza kwamba mwenge huo pia utazindua miradi minne yenye thamani ya shilingi milioni 79,160,000 .Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi  wakati mwenge wa uhuru utakapokuwa unazindua , kufungua na kuwekea mawe ya msingi katika maeneo yao .

Mwenge wa uhuru unatarajia kuanza kukimbizwa katika Mkoa huo tarehe 5 ya mwezi huu.

No comments:

Post a Comment