HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 4 March 2014

WATU WATATU APOTEZA MAISHA MKOANI IRINGA KATIKA MATUKIO TOFAUTI "mmoja apigwa risasi"


RPC MUNGI 


Na  Diana Bisangao wa matukiodaima.com Iringa 
..................................................................................
WATU  watatu wafariki dunia mkoani Iringa katika matukio manne tofauti likiwemo la mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Zawadi Mlaso(35) mkazi wa Mahenge wilaya ya Kilolo kufariki dunia baada ya kupigwa risasi.

Akizungumza na wanahabari ofisini kwake Kamanda wa polisi mkoani Iringa Ramadhani Mungi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea mnamo tarehe 2 machi majira ya saa 3:30 usiku.

Kamanda Mungi alisema marehemu alipigwa maeneo ya shingoni na silaha aina ya gobore linalotumia goroli hata hivyo watu waliompiga hawajafahamika na chanzo cha tukio bado kinachunguzwa.

Katika tukio lingine mtu mmoja jina Richard Leonard (29) mchimbaji wa madini eneo la Saadan alifariki dunia baada ya kutumbukia kwenye shimo la madini lenye urefu wa futi 50.

Kamanda alisema tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 28 februari majira ya saa 2 kamili usiku katika machimbo ya madini ya Ihazutwa wilaya ya Mufindi ambapo marehemu alifariki papo hapo baada ya kutumbukia.

Mtu mmoja jina Thobias Mwangunguro (32) mchimbaji wa madini maeneo ya Ulata, kata ya Kiponzero wilaya ya Iringa Vijijini alifariki dunia wakati akikimbizwa Hospitali ya Wilaya ya Mafinga.

Kamanda alisema tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 28 februari majira ya saa 10 kamili alfajiri na kusema marehemu alipata ajali ya kutumbukia kwenye shimo la madini na kupata maumivu makali.

Mbali na matukio hayo matatu ya vifo Kamanda Mungi alisema JESHI la polisi mkoani hapa linamshikilia Fadhil Mahimba (20) mkazi wa Gangilonga kwa kosa la kukutwa na misokoto 40 ya bangi. 

No comments:

Post a Comment