HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 26 March 2014

HABARI ZA KIMICHEZO KUTOKA MAJUU



CHELSEA KUTENGA ZAIDI YA EURO MILIONI 36 KWA AJILI YA DIEGO COSTA.




KLABU ya Chelsea imeanza mikakati ya kumnasa mshambuliaji nyota wa Atletico Madrid, Diego Costa katika kipindi cha usajili majira ya kiangazi. Vinara hao wa Ligi Kuu wako tayari kutoa zaidi ya euro milioni 36 kwa ajili ya mshambuliaji huyo. Tayari wawakilishi wa Chelsea wameshaomba kukutana na kambi ya Costa na mazungumzo zaidi yanatarajiw akufanyika wiki ijayo. Chelsea wamepania kumnasa nyota huyo kabla ya kumalizika kwa msimu wa ligi na kuanza kwa michuano ya Kombe la Dunia ambayo anatarajiwa kuiwakilisha Hispania kutetea taji lao. Costa mwenye umri wa miaka 25 tayari amefunga mabao 31 katika mechi 41 alizocheza msimu huu katika mashindano yote huku akimfuatia Ronaldo mwenye mabao 26 kwa ufungaji wa mabao kwenye La Liga akiwa na mabao 23.

SIJAWAHI KUWAFUNDISHA XAVI NA INIESTA KUCHEZA SOKA - GUARDIOLA.
 
MENEJA wa klabu ya Bayern Munich, Pep Guardiola amedai kufanya machache kuwageuza nyota wa Barcelona Xavi na Andres Iniesta kuwa wachezaji bora duniani. Viungo hao wa kimataifa wa Hispania wakiwa chini ya Guardiola alipokuwa Camp Nou waliiwezesha timu hiyo kunyakuwa mataji 14 kutoka mwaka 2008 mpaka 2011, yakiwemo mataji mawili ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya. Xavi na Iniesta pia walikuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Hispania kilichonyakuwa mataji ya Ulaya sambamba Kombe la Dunia, na Guardiola amedai kuwa wachezaji wa aina hiyo hawahitaji kocha ili wacheze katika kiwango bora. Guardiola amesema wachezaji wa Barcelona wanajipa msukumo wenyewe, hajawahi kuwafundisha Xavi na Iniesta kucheza soka kazi yake ilikuwa ni kutoa msaada wa kiufundi kwani wamekuwa wakicheza vyema kwa miaka 20.

MASHABIKI WAMGEUKA FERGUSON KWA KUWACHAGULIA BOMU MOYES. 

 

MASHABIKI wa klabu ya Manchester United wamemgeukia kocha wa zamani wa timu hiyo Sir Alex Ferguson baada ya kuona wakipokea kipigo kutoka mahasimu wao Manchester City katika Uwanja wa Old Trafford jana usiku. City ambao waliwasambaratisha majirani zao hao kwa mabao 3-0 yaliyofungwa na Edin Dzeko na Yaya Toure, waliamsha hasira kwa mashabiki hao na kuanza kuonyesha mabango ya kumlaumu Ferguson ambaye ndiye aliyemchagua David Moyes kuchukua nafasi yake. Mbali na kumshambulia Ferguson lakini pia kulikuwa mabango mbalimbali ya kumpinga Moyes kwenye mchezo huo. Hasira za mashabiki hao zimeibuka kutokana na timu hiyo kushindwa kufanya vyema msimu huu hususani katika uwanja wao wa nyumbani.

No comments:

Post a Comment