HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Saturday, 22 February 2014

TAZAMA COASTAL WALIVYO IKALISHA MBEYA CITY LEO 2-0


MASHABIKI WA MBEYA CITY


DANNY LAYNGA WA COASTA AKIMILIKI MPIRA


WACHEZAJI WA COASTA UNION WAKIMPONGEZA MOHAMMED MIRAJI(10) KWA BAO SAFI

BOBAN AKIWA DIMBAN LEO

MASHABIKI WA COASTAL UNION

Hatimaye wabishi wa Mbeya City wamekubali kipigo cha pili katika Ligi Kuu Bara baada ya kufungwa bao 2-0 na wenyeji Coastal Union. kwa Bao za Chipukizi Mohamed Miraji aliefunga katika Dakika ya 80 na 92 na kuifanya Coastal kufikisha pointi 25 na kuikamata Ruvu Shooting.

Mchezo huo ambao ulianza kwa kasi kwa timu zote kushambuliana kwa zamu ambapo mpaka timu zote zinakwenda mnapumziko hakuna timu iliyoweza kuona lango la mwenzie.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kwa timu zote kuingia uwanjani hapo zikiwa zimefanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji wake ambapo kwa upande wa Coastal Union waliwatoa Ally Iddy,Crispian Odulla na Ayoub Yahaya ambao nafasi zao zilichukuliwa na Suleimani Selembe,Mohamed Mtindi,Yayo Lutimba na Keneth Masumbuko.

Kwa upande wa Mbeya City waliwatoa Mwegane Yeya,Jeremia John nafasi zao zilichukuliwa na Fransisi Casto na Richard Peter ambao waliweza kucheza vema licha ya kushindwa kuibuka na ushindi kwenye mechi hiyo.

Vikosi vilivyozeshwa leo kwa upande wa Coastal Union iliwachezesha Shabani Kado,mbwana hamisi,abdi banda,juma nyoso,yusuph chuma,jerry santo,Daniel lyanga,ally iddi,haruna moshi,crispian odulla na ayoub yahya.

Kwa upande wa Mbeya City iliwachezesha Davidi buruani,azizi sibo,hasan mwasapili,deogratis Julius,yusuph abdallah,Anthony matogolo,mwagane yeya,steven mazand,paul nonga,jeremia john na peter mapunda.

No comments:

Post a Comment