HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Sunday, 23 February 2014

SIMBA HOI KWA JKT RUVU, AZAM YABANWA, YANGA NAMBARI WANI!



>>>MNYAMA HOOI KWA MAAFANDE
VPL, Ligi Kuu Vodacom, iliendelea Leo kwa Mechi mbili Jijini Dar es Salaam ambapo Azam FC ilibanwa kwa Sare ya 2-2 walipocheza na Tanzania Prisons, Matokeo ambayo yamewafanya Mabingwa Yanga waendelee kubaki kileleni, na Simba kukiona cha mtema kuni walipochapwa Bao 3-2 na JKT Ruvu.
++++++++++++++++++++++++++
LIGI KUU VODACOM
MATOKEO:
Jumapili Februari 23
Simba 2 JKT Ruvu 3
Azam FC 2 Tanzania Prisons 2
++++++++++++++++++++++++++
Kocha wa Simba Zdravko Logarusic
SIMBA 2 JKT RUVU 3
Kwenye Mechi iliyochezwa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam JKT Ruvu Leo iliwaendesha mchakamchaka Simba na kuwanyuka Bao 3-2.
Hadi Mapumziko, JKT Ruvu walikuwa mbele kwa Bao 2-0 zilizofungwa na Hussein Bunu na Penati ya Emmanuel Swita ambayo waliipata baada Henry Joseph kumchezea rafu Amos Mgisa.
Katika Dakika ya 53, Emmanuel Swita aliifungia JKT Ruvu Bao la 3 na kuwafanya waongoze 3-0 lakini Simba walicharuka na kupata Bao mbili zilizofungwa na Amisi Tambwe Dakika ya 64 na 84, moja likiwa kwa Penati baada ya Bunu kumuangusha Amri Kiemba.
JKT Ruvu, licha ya kumaliza Mtu 10 baada ya Damas Makwaya kupewa Kadi Nyekundu kwenye Dakika ya 72 baada Kadi za Njano mbili, walisema kidete na kulinda ushindi wao.
Logaruzic akiwa na Wachezaji Maozezini

Patashika kwenye lango la JKT Ruvu

Tambwe akimtoka Beki wa JKT Ruvu

Mashabiki wa Simba wakiwa hawaamini kinachotokea

VIKOSI:
SIMBA: Yaw Berko, William Lucian 'Gallas', Henry Joseph,  Joseph Owino, Donald Mosoti, Jonas Mkude, Awadh Juma, Said Ndemla, Amissi Tambwe, Amri Kiemba, Haruna Chanongo.
JKT RUVU: Shaaban Dihile,  Damas Makwaya, Edward Charles, George Minja, Salum Mtaki, Nashon Naftali, Amos Mgisa, Emmanuel Swita, Idd Mbaga, Hussein Bunu, Sosthenes Manyasi

++++++++++++++++++++++++++ 

AZAM FC 2 PRISONS 2
Huko Azam Complex, Chamazi, kwenye Viunga vya Jiji la Dar es Salaam, Wenyeji Azam FC waliikosa nafasi ya kutwaa uongozi wa Ligi toka kwa Yanga baada kutoka Sare ya 2-2 na Tanzania Prisons.
Hadi Mapumziko Bao zilikuwa 0-0.
Prisons ndio waliofunga Bao la Kwanza katika Dakika ya 47 kwa Frikiki ya Omega Seme na Azam kusawazisha chapchap katika Dakika ya 49 kwa Bao la Aggrey Morris na kupiga Bao la Pili Dakika moja baadae kwa Bao la Kipre Tcheche.
Haikuchukua muda kwa Kipre Tcheche kupewa Kadi ya Njano ya Pili na hivyo kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu na hii iliwapa mwanya Prisons ambao hatimae kwenye Dakika ya 80 walisawazisha kwa Bao la Mpalile.
Benchi la Ufundi la Azam(Kalli Ongalla kushoto na Joseph Marius Omog)

VIKOSI:
AZAM FC: Mwadini, David, Erasto, Moradi, Aggrey Morris, Bolou, Himidi, Abubakar Sure Boy, John Bocco, Brian Omony, Kipre Tchetche
Akiba: Aishi, Jabir, Mwaipopo, Mcha, Kone, Malika, Kelvin
TANZANIA PRISONS: Wilbeth Mweta, Salum Kimenya, Lauriun Mpalile, Nurdin Chona, Lugano Mwangama, Jimmy Shoji, Godfrey Magetha, Omega Seme, Peter Michael, Frank Wiliam Muwi, Fred Chudu .
Akiba: Beno Kakolanya, Bryson Mponzi, Henry Mwalugala, Hamisi Maingo, Six Ally Mwasekaga, Jumanne Elfadhili, Ibrahimu Isihaka.
RATIBA:
Jumatano Februari 26
Azam FC v Ashanti United
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
GD
PTS
1
Yanga SC
17
11
5
1
29
38
2
Azam FC
17
10
7
0
19
37
3
Mbeya City
19
9
8
2
8
35
4
Simba SC
19
8
8
3
16
32
5
Kagera Sugar
19
6
8
5
1
26
6
Coastal Union
19
5
10
4
5
25
7
Mtibwa Sugar
19
6
7
6
0
25
8
Ruvu Shooting
18
6
7
5
-4
25
9
JKT Ruvu
19
7
1
11
-13
22
10
Prisons FC
17
3
8
6
-3
17
11
Mgambo JKT
19
4
5
10
-17
17
12
Ashanti United
18
3
5
10
-15
14
13
JKT Oljoro
19
2
8
9
-15
14
14
Rhino Rangers
19
2
7
10
-11
13

No comments:

Post a Comment