HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 19 February 2014

CHAMPIONS LEAGUE VILIO SASA NI KWA TIMU ZA NYUMBANI "click hapa kwa taarifa zadi"



Thursday, 20 February 2014 00:48
>>MTINDO MPYA ULAYA: TIMU ZA NYUMBANI HOI KWA SIKU YA PILI!
UEFA CHAMPIONZ LIGI
MATOKEO:
Jumatano Februari 19
AC Milan 0 Atletico de Madrid 1
Arsenal FC 0 Bayern Munich 2

++++++++++++++++++++++++++++++++++++


ARSENAL 0 BAYERN MUNICH 2
Kwenye Mechi ambayo Kipindi cha Kwanza kilishuhudia Penati mbili kukoswa na Kadi Nyekundu, Mabingwa Watetezi Bayern Munich wamefanikiwa kuichapa Arsenal waliokuwa kwao Emirates Bao 2-0 katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI.

Dakika ya 8 Mesut Ozil aliangushwa na Boateng na Penati kutolewa lakini Penati hiyo iliyopigwa hafifu na Ozil iliokolewa na Kipa Manuel Neuer ambae ni Rafiki wa Ozil tangu utotoni.
Kwa Ozil hiyo ni Penati yake ya Tatu mfululizo kukosa akichezea Klabu, nyingine zikiwa Arsenal ilipocheza na Marseille kwenye Makundi ya UCL Msimu huu na kabla wakati akiwa na Real Madrid.

Kwa kawaida Wapiga Penati wa Arsenal ni Olivier Giroud na Mikel Arteta na wote hawakuwamo kwenye Mechi hii.
Kwenye Dakika ya 37 Toni Kroos alipenyeza pasi ya juu kwa Arjen Robben ambae alichomoka na kuipita Difensi na kukontroli Mpira akimhadaa Kipa Wojciech Szczesny ambae alimwangusha na Refa Nicola Rizzoli toka Italy kutoa Penati na Kadi Nyekundu kwa Szczesny.

Lakini David Alaba alikosa Penati hiyo iliyopiga Posti chini na kutoka huku Kipa wa Akiba, Fabianski, alieingizwa baada kutolewa Santi Cazorla ili kukaa langoni ‘akienda mbovu’.
Katika Dakika ya 54, baada kupokea pasi safi toka kwa Nahodha Philip Lahm, Toni Kroos aliachia shuti toka Mita 20 ambalo lilipita juu kulia na kutinga wavuni na kuwapa Byern Munich Bao safi.

++++++++++++++++++++++++++++++++++++
TAKWIMU MUHIMU-Toni Kroos v Jack Wilshere
-TONI KROOS: Pasi 152, 127 ndani ya Nusu ya Uwanja upande wa Arsenal, ikiwa ni Asilimia 96.7% ya Pasi zilizokamilika sahihi.
-JACK WILSHERE: Pasi 33, Asilimia 66.7% sahihi.
++++++++++++++++++++++++++++++++++++

Bayern katika Dakika ya 88 baada ya pasi yake kuunganishwa kwa kichwa kilichodunda chini cha Thomas Muller, alieingia Kipindi cha Pili, na kumhadaa Kipa Fabianski.
Kwa ushindi huu wa Bao 2-0, Mabingwa wa Ulaya Bayern Munich wamejiweka katika hali njema kucheza Robo Fainali na Arsenal wanahitaji kushinda 3-0 huko Munich ili wapindue kipigo.
Timu hizi zitarudiana huko Allianz Arena Jijini Munich, Germany hapo Machi 11.

VIKOSI:
ARSENAL (Mfumo 4-2-3-1): Szczesny, Sagna, Mertesacker, Koscielny, Gibbs; Flamini, Wilshere; Ozil, Cazorla, Oxlade-Chamberlain; Sanogo.
Akiba: Fabianski, Rosicky, Podolski, Giroud, Monreal, Jenkinson, Gnabry.
BAYERN MUNICH (Mfumo: 4-1-2-3): Neuer; Boateng, Dante, Martinez, Alaba; Lahm; Thiago, Kroos; Robben, Mandzukic, Gotze.
Akiba: Starke, Van Buyten, Rafinha, Pizarro, Muller, Contento, Schweinsteiger.
Refa: Nicola Rizzoli (Italy)

++++++++++++++++++++++++++++++++++++

AC MILAN 0 ATLETICO MADRID 1
Bao la Dakika ya 82 kwa kichwa cha Straika hatari Diego Costa limewapa Atletico Madrid ushindi wa Bao 1-0walipocheza Ugenini huko San Siro na AC Milan katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Timu hizi zitarudiana huko Estadio Vicente Calderon hapo Machi 11.
VIKOSI:
AC MILAN (Mfumo 4-2-3-1): Abbiati, De Sciglio, Bonera, Rami, Bonera, Emanuelson; Essien, De Jong; Poli, Kaká, Taarabt; Balotelli.
Akibas: Amelia, Mexès, Abate, Constant, Zaccardo, Pazzini, Petagna.
ATLÉTICO MADRID [Mfumo 4-4-2]  : Courtois, Juanfran, Godín, Miranda, Insua; Gabi, Mario Suárez; Koke, Raúl García, Arda Turan; Diego Costa.
Akiba: Aranzubia, Alderweireld, Cristian Rodríguez, Sosa, Diego, Adrián López, Villa.

Refa: Proença (Portugal)  
UEFA CHAMPIONZ LIG
Raundi ya Mtoano ya Timu 16
MATOKEO:
Jumanne Februari 18
Manchester City 0 FC Barcelona 2
Bayer 04 Leverkusen 0 Paris Saint-Germain 4 
RATIBA:
[Saa za Bongo]
Jumanne Februari 25
20:00 Zenit St. Petersburg v BV Borussia Dortmund
22:45 Olympiacos CFP v Manchester United
Jumatano Februari 26
22:45 Schalke 04 v Real Madrid CF
22:45 Galatasaray Spor Kulübü v Chelsea FC
MARUDIANO
Jumanne Machi 11
22:45 Bayern Munich v Arsenal FC
22:45 Atletico de Madrid v AC Milan
Jumatano Machi 12
Jumatano Machi 12
22:45 FC Barcelona v Manchester City
22:45 Paris Saint-Germain v Bayer 04 Leverkusen
Jumanne Machi 18
22:45 Chelsea FC v Galatasaray Spor Kulübü
22:45 Real Madrid CF v Schalke 04
Jumatano Machi 19
22:45 BV Borussia Dortmund v Zenit St. Petersburg
22:45 Manchester United v Olympiacos CFP
++++++++++++++++++++++++++++++++++

No comments:

Post a Comment