HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Sunday, 19 January 2014

POMBE HARAMU YAENDELEA KUSHAMIRI DAR





Na Keneth JOhn  wa matukiodaima.com ,Dar
Biashara  ya  pombe  haramu  aina  ya   gongo    imeendelea  kushamili  jijini  Dar  es  salaam   baada  ya  jeshi  la  polisi  kanda  maalum  ya  dar  es  salaam  kukamata  lita  58  za   pombe  hiyo  kwa  nyakati  tofauti.

Taarifa  kutoka  jeshi   la  polisi   kanda  maalumu  ya  Dar  es  salaam zinasema  kuwa  jan  18  majira  ya  saa  5  kamili  asubuhi  maeneo  ya  Bunju  “A”   mbweni  kata  ya  mbweni  mbezi  beach,  askari  walifanya  msako  maeneo  hayo  na  kufanikiwa  kuwakamata  watuhumiwa  6  ambao  ni  Pili  Rajabu (50) Hamisi  Kilie  (41) Hamuisi  Kasimu(45) na  wenzao  wengine  watatu  wakiwa  na  pombe  haramu  ya  gongo  lita  40  pamoja  na  bhangi  kete  122 .

Pamoja  na  hayo   jan  18  hiyo  hiyo  askari   pia  walipitisha  msako  mkali  maeneo  ya  Kibamba  kata  ya  kibamba  kimara  stop  over,  na  kufanikiwa  pia  kuwakamata  watuhumiwa  23  ambao  ni  Maneno  Adamu  (20)  Rajabu  Omary  (25)  na  Mwajuma   Juma  (25)  pamoja  na  wenzao  20   wakiwa  na  pombe  haramu  aina  ya  gongo  lita  18  pamoja  na  bhangi  puli  12 ,  kete  25  na  misokoto  70.

No comments:

Post a Comment