HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 10 December 2013

TANESCO YAKANUSHA MADAI YA BAADHI YA VYOMBO VYA HABARI


Meneja Uhusiano wa shirika hilo Badra Masoud

Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) Limekanusha taarifa iliyotolewa na baadhi ya habari kuwa liko mbioni kufikishwa mahakama kutokana na kuvunja mkataba na kampuni ya McDonald Live Line Technology Limited.

Akikanusha taarifa hiyo Meneja Uhusiano wa shirika hilo Badra Masoud amesema kuwa shirika liliamua kuvunja mkataba na kampuni hiyo baada ya kushindwa kutekeleza zabuni waliyopewa ya kusafirisha, kusambaza na kuweka nguzo za umeme katika eneo la Kiyungi/Arusha 06 kV lines iliyotakiwa kukamilika ndani ya wiki 32 kuanzia Julai 28, 2010 na kuisha mwezi Machi 11, 2011.

Badra aliongeza kuwa baada ya mkataba huo kuvunjwa kampuni ya McDonald ilifungua shauri katika Tume ya Usuluhishi na Ushindani ambapo mara baada ya pande zote kusikilizwa kampuni hiyo iliamriwa kuilipa TANESCO fidia ya zaidi ya milioni 700.

No comments:

Post a Comment