HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 12 December 2013

PATA HABARI YA ZITTO" SASA AAMUA KUKATA RUFAA HUKUMU YAKE CHADEMA


Zitto Kabwe

MGOGORO wa uongozi ndani ya Chadema, sasa umehamishiwa rasmi Baraza Kuu kwenye mpasuko, baada ya watuhumiwa waliovuliwa madaraka na Kamati Kuu (CC) ya chama hicho, kukata rufaa huko wakijua kuna wapinzani waliojitokeza hadharani dhidi ya CC na Mwenyekiti Freeman Mbowe.

CC ya Chadema, iliwavua madaraka Naibu Katibu Mkuu na Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Zitto Kabwe, Mjumbe wa CC, Dk Kitila Mkumbo na Mwenyekiti wa Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.
Chama hicho kilidai kuwa hatua hiyo ilitokana na usaliti na njama za kutaka kufanya mapinduzi, huku wenyewe wakijitetea hadharani kuwa walitaka kumtumia Zitto, agombee uenyekiti wa Taifa dhidi ya Mbowe, ambaye anatajwa kutaka kuutetea. Jana mwanasheria wa watuhumiwa hao, Albert Msando, alitangaza hatua iliyochukuliwa na viongozi hao, kwamba ni kupinga uamuzi wa CC kwa Baraza Kuu.

“Kuna sababu mbili za msingi za kukata rufaa; kwanza utaratibu wa kuchukua hatua za nidhamu ulikiukwa, na pili, sababu za kuchukuliwa hatua hizo si sahihi,” alisema Msando, ambaye alipata kuwa wakili wa Mbowe. Moto Baraza Kuu Hatua ya akina Zitto ilitarajiwa na wengi kwa kuwa baada ya uamuzi huo wa Kamati Kuu, Dk Mkumbo, ambaye ndiye aliyeandika Ilani ya Uchaguzi ya Chadema, alikubaliana nao lakini aliukosoa.
“Kwa mujibu wa Katiba ya Chadema, Sura ya Sita, Ibara ya 6.3.6 (b); ‘kiongozi aliyeteuliwa na vikao vya juu vya uongozi atasimamishwa au kuachishwa uongozi na kikao kilichomteua.
“Mimi nilichaguliwa na Baraza Kuu na ni kikao hiki pekee chenye uwezo wa kunivua nafasi niliyonayo. Ninaamini wajumbe wa CC walipitiwa katika hili, kwa sababu siamini kwamba hawajui matakwa haya ya kikatiba, ukizingatia kwamba ndani yake kuna wajumbe waliobobea kabisa katika tasnia ya sheria,” alisema.
Mbali na kauli hiyo ya Dk Mkumbo, msomi ambaye alikuwa pia mwandishi wa hotuba za mgombea urais wa Chadema mwaka 2010, Dk Willibrod Slaa, baadhi ya wajumbe wa Baraza walijitoa mhanga kumwunga mkono Zitto na kuipinga CC hadharani, huku wakimtaka Mbowe aitishe kikao cha dharura cha Baraza Kuu.
Kanda ya Dar es Salaam Mjumbe wa kwanza kufanya hivyo, alikuwa Patrick Joseph, Mjumbe wa Baraza Kuu pamoja na vyeo vingine, ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Baraza la Vijana la Taifa (Bavicha).
“Nimefadhaishwa sana na uamuzi uliofikiwa na CC ya chama dhidi ya Zitto na Dk Mkumbo mbali na kwamba CC haikuwa na mamlaka ya kikanuni wala kikatiba kufikia uamuzi ilioufikia na kuutangaza kwa umma.
“Msimamo wangu, namtaka Mwenyekiti (Mbowe) akishirikiana na watendaji wengine wa chama waitishe mkutano wa dharura wa Baraza Kuu, ili tutoe uamuzi sahihi wa suala hili.

“Ninataka pia pamoja na ajenda zitakazojadiliwa, watueleze ni kwa nini tusiamini kwamba uamuzi huu umeathiriwa na hofu ya uchaguzi ndani ya chama. Ni kitu gani kimeifanya Sekretarieti ya CC itangaze ratiba ya Uchaguzi Mkuu baada ya kuchafua watu waliotarajiwa kugombea nafasi mbali mbali mpaka kuwavua uanachama?” alihoji Joseph.
Kanda ya Kusini Wajumbe wengine kujitoa mhanga ni Ally Chitanda, aliyekuwa Mwenyekiti wa Mkoa wa Lindi, Kanda ya Kusini na Katibu wa Sekretarieti ya CC. Katika taarifa yake, alisema:
“Ningependa kuwaambia wana Chadema na Watanzania kwa ujumla, uamuzi huu wa Kamati Kuu wa kuwavua uongozi Zitto na Dk Mkumbo ni wa kijuha na unaofanya Watanzania sasa waangalie mara mbili mbili kama hawa watu wako makini na huo ukombozi wanaousema.”
Kanda ya Kati, Kigoma Kutoka Kanda ya Kati, Mjumbe wa Baraza Kuu na aliyekuwa Mwenyekiti wa Mkoa, Wilfred Kitundu alijiuzulu nafasi yake na kubaki na ujumbe wa Baraza.
“Tunalaani, kupinga na kukemea CC ya chama dhidi ya uamuzi wao huu uliojaa chuki, hofu na wasiwasi mwingi kuelekea uchaguzi mkuu ndani ya chama.
“Tunamtaka Mwenyekiti na Katibu Mkuu, waitishe mara moja mkutano wa Baraza Kuu la chama kutolea uamuzi suala hilo. Kigoma, Mjumbe wa Baraza Kuu na Mwenyekiti wa Mkoa, Jafari Kasisiko, alisema:
“Maoni ya wengi mkoani na viongozi wa chama ni kuudhiwa na uamuzi ya CC ambao dhahiri ulilenga kummaliza Zitto kisiasa.” Kwa Msajili Mbali na kukata rufaa Baraza Kuu, Mwigamba alikwenda mbali zaidi kwa Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, kushitaki alichoita ni kuchezewa kwa Katiba ya Chama.
“Nitaomba (Msajili) atoe mwongozo kuhusu mgogoro wa kikatiba ndani ya chama unaotokana na kipengele cha Katiba kinachogusia ukomo wa uongozi kubadilishwa kinyume na utaratibu,” alisema Mwigamba. Mwigamba anadai kuwa Katiba ya 2004, kipengele 5.3.2 (c) kinachosomeka:
“Muda wa Uongozi: Kiongozi aliyemaliza muda wa uongozi, ana haki ya kugombea na kuchaguliwa tena, ili mradi awe anatimiza masharti ya kuchaguliwa kuwa kiongozi kwa muda usiozidi vipindi viwili katika cheo kimoja kwa ngazi moja. Katiba ya sasa ya mwaka 2006, kipengele cha 6.3.2 ( c) kinachozungumzia muda wa uongozi kinasomeka: “Kiongozi aliyemaliza muda wa ungozi, ana haki ya kugombea na kuchaguliwa tena, ili mradi awe anatimiza masharti ya kuchaguliwa kuwa kiongozi.”
Mwigamba anadai maneno ‘kwa muda usiozidi vipindi viwili katika cheo kimoja kwa ngazi moja’, yaliondolewa kinyemela wakati wa kuchapisha Katiba hiyo.

Anakiri ni kweli kuwa marekebisho ya Katiba yalifanyika mwaka 2006, lakini hoja ya kubadili kipengele hicho haikuwapo na mihutasari inaonesha wazi hakukuwa na mjadala wa kipengele hicho au kuhusu suala zima la ukomo wa uongozi.

Kama hoja hiyo ikipita na kukubaliwa na Msajili, Mbowe atakuwa amepoteza haki ya kutetea nafasi yake kama Mwenyekiti wa Taifa, kwa kuwa ameshaongoza kwa vipindi viwili na kumpa nafasi Zitto ambaye alishaonesha nia siku nyingi ya kuitaka nafasi hiyo.
Kama hoja hiyo ikikosa mashiko kwa Msajili, Mbowe atakuwa na fursa ya kutetea kiti hicho kwa mara ya tatu, na atakuwa Mwenyekiti wa kwanza kufanya hivyo kwa kuwa huko nyuma Katiba haikuruhusu.
Chanzo ;

Habari Leo

No comments:

Post a Comment