HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 17 December 2013

JESHI LA POLISI MKOANI ARUSHA LAKAMATA SH MIL 60 BANDIA KWA USHIRIKANO NA WANANCHI


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Liberatus Sabas akiwaonyesha waandishi wa habari (Hawapo pichani) noti bandia zenye thamani ya Tsh 6,140,000 ambazo zilikamatwa maeneo ya Kituo kikuu cha Mabasi cha jijini hapa ambapo mtuhumiwa alikuwa anataka kuzisafirisha kwenda Dar es salaam. (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha)


Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha
Jeshi la Polisi Mkoani hapa limemkamata mwanamke mmoja aitwaye Imelda Juma (20) Mkazi wa Sokoni One jiji hapa akiwa na noti bandia zenye thamani ya Tsh 6,140,000 (Milioni sita laki moja na elfu orobaini).
Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Liberatus Sabas alisema kwamba tukio hilo lilitokea tarehe 13.12.2013 muda wa saa 10:00 Alasiri katika maeneo ya Kituo kikuu cha Mabasi mara baada ya jeshi hilo kupata taarifa toka kwa raia wema.

Kamanda Sabas alifafanua kwa kusema kwamba, siku ya tukio mtuhumiwa ambaye ni Imelda Juma alimtuma dereva wa pikipiki maarufu kama “boda boda” aitwaye Jamal Abdul ili aende maeneo ya Sakina Darajani kwenda kuchukua mzigo. Mara baada ya dereva huyo kufika katika eneo hilo aliukuta mzigo huo ukiwa pembeni ya pikipiki nyingine ambayo haikuwa na mtu.
Dereva huyo wa pikipiki aliuchukua mzigo huo na kuupeleka katika kituo cha mabasi cha Dar Express kama alivyoelekezwa na mtuhumiwa ambaye ndio mmiliki wa mzigo huo ili autume kwa mtu aliyefahamika kwa jina moja la Emmanuel ambaye inadaiwa yupo Dar es salaam.
Wafanyakazi wa kampuni ya mabasi ya Dar Express waliokuwa ofisini hapo hawakuwa tayari kuupokea na kuusafirisha mzigo huo bila kuufungua ili wajiridhishe japokuwa dereva wa boda boda alikataa kufungua mzigo huo kwa madai kwamba mwenye mzigo alimwambia hasikubali mzigo huo ufunguliwe.

“Ndipo wafanyakakazi hao wakamshauri dereva huyo wa boda boda kama hataki ufunguliwe basi naye pia akate tiketi ili asafiri pamoja na mzigo wake mpaka Dar es salaam”. Alisema Kamanda Sabas.
Mara baada ya taarifa hiyo kufika katika kituo kikuu cha Polisi, askari waliweka mtego na kumkamata mtuhumiwa huyo Imelda Juma ambaye inasemekana alikuwa maeneo ya karibu na hapo.

Mpaka hivi sasa Jeshi hilo linaendelea kumhoji mtuhumiwa huyo ili kuweza kubaini mtambo unaotengeneza fedha hizo bandia huku pia likiendelea kumtafuta mtumiwa mwingine aitwaye Emmanuel.
Kufuatia tukio hilo Kamanda Sabas ameendelea kuwashukuru wananchi wa Mkoa huu kwa jinsi wanavyoshirikiana na jeshi hilo juu ya utoaji wa taarifa kwani fedha hizo kama zingesambaa mtaani kwa ajili ya matumizi zingedhoofisha uchumi wa nchi kwa kiasi fulani.
Aidha amewatahadhalisha wananchi wa Mkoa huu hasa wafanyabiashara kuwa makini na noti mbalimbali wanazozipokea toka kwa wateja wao, kwani wengine hutumia mwanya wa wingi wa noti kupenyeza fedha bandia.

No comments:

Post a Comment