HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 2 December 2013

CHUO KIKUU HURIA KITUO CHA MKOA WA TANGA CHAKOSA USHIRIKIANO KUTOKA KWA TAASISI ZA SERIKALI





Na Godwin Lyakurwa Tanga
 Taasisi za Serikali na zisizo za Kiserikali Mkoani Tanga zimetakiwa kutoa ushirikiano wa kutosha katika Masuala yanayohusu Utafiti,Ushauri na Elimu kwa Chuo Kikuu Huria Kituo cha Mkoa wa Tanga ili kuweza kufanikisha shughuli za kimaendeleo kwa urahisi zaidi Mkoani hapa.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi wa Chuo Hicho Bi RAHMA MOHAMMED wakati akizungumza na Wanahabari Dec29 Chuoni  hapo, ambapo ameeleza kuwa Chuo hicho kimekuwa hakipewi hadhi na Ushirikiano wa kutosha kutoka kwa wanajamii na Taasisi mbalimbali Mkoani hapa.

Akielezea Historia ya Chuo hicho Bi Rahma amesema kuwa kilianzishwa kama moja kati ya zaidi ya vituo 30 vya Chuo kikuu Huria cha Tanzania vilivyoko nchini , ambapo kilianzishwa Mwaka 2000 katika majengo Veta kikiwa na wanafunzi 53 hadi 1005 mwaka huu wa masomo 2013/2014 ambapo tangu mwaka 2018 mpaka sasa kinafanya shughuli zake katika majengo ya TUKTA jijini Tanga.

Akielezea mafanikio ya Chuo hicho Bi Rahma ameeleza kuwa Chuo kimefanikwa kudahili wanafunzi kutoka 53 mpaka 1001 kwa mwaka 2000/2013.Pia kimefanikiwa kuongeza wahitimu kutoka 53 kwa mwaka 2011 mpaka 101 kwa mwaka 2013.

Kwa upande wa Kafanikio amesema kuwa Chuo kimefanikiwa kuanzisha Vituo katika Wilaya zote za Mkoa wa Tanga, Chumba maalum cha Computer chenye Computer 10 zilizounganishwa kwenye Mtandao wa Enternet ambapo wanafunzi huweza kujisomea na kupata taarifa kwa njia ya mtandao bure,kuongeza miundombinu ya kutoa taaluma bora kupitia michango ya wanafunzi kama Viti 40 na kujenga banda la kusomea wanafunzi.

Aidha Mkurugenzi huyo amebainisha Changamoto mbalimbali zinazo kikabili chuo hicho kuwa ni pamoja na Ardhi kwa Ajili ya kujenga Majengo maalum yatakayokuwa mali ya Chuo hicho.

“Tunachangamoto ya uhaba wa Ardhi kwa ajili ya kujenga Majengo yetu Wenyewe ambapo tuliomba eneo na kupewa Eneo Wilaya ya Muheza katika Eneo la Kilapura lakini lilivamiwa na Wanachi kabla hatujamilikishwa hivyo Halmashauri ya Wilaya ya Muheza  ikatukahamisha katika eneo jingine lililoko Kibanda na tnasubiri Taratibu za kukabidhiwa”Alisema Bi Rahma.

Hata hivyo Mkurugenzi huyo ameeleza kuwa bado si bora sana kupata eneo nje ya mji kwa sababu itakuwangumu kupata mawasiliano kutoka Mkongo wa mawasiliano wa Taifa.

Akielezea Changamoto nyingine Bi Rahma amesema kuwa uelewa finyu kwa Wananchi walioko mkoani Tanga hasa kwa kufikiri kuwa Taaluma inayotolewa Chuoni hapo kuwa si nzuri kama ile inayotoka katika vyuo vya bweni kitu ambacho si kweli, hali ambayo imesababisha Chuo hicho kushindwa kufikia Malengo ya Udahili mwaka hadi mwaka.

Amesema pia uhaba wa kifedha kwa ajili ya kufika katika maeneyo ya Vijijini kwa ajili ya kuwaelimisha na kuwatangazia wanachi juu ya Ubora wa kutumia Chuo kikuu Huria kituo cha Mkoa wa Tanga.

Bi Rahma amesema kuwa hali hiyo imepelekea baadhi ya Kozi zinazotolewa Chuoni hapo kutotambulika na baadhi ya Taasisi za Kiserikali Mkoani hapa akitolea Mfano Walimu zaidi ya 30 waliohitimu Kozi ya Diploma Kituoni hapo na wanafanya kazi Wilayani Tanga mwajiri wao(TSD) amekataa kuwapandisha madaraja na kuwataka warejeshe Barua walizochukua kwa ajili ya kupandishwa Daraja kwa sababu ya kutoitambua kozi hiyo jambo ambalo linashangaza na linarudisha nyuma maendeleo ya Chuo hicho kwa baadhi ya wanafunzi wanaosoma kozi hizo kwa sasa kujitoa katika Kozi hiyo.

Nae Raisi wa Chuo hicho EUSTARD RWEGOSHORA mesema kuwa wanashukuru Uongozi wa Chuo hicho kwa Ushirikiano mkubwa walionao kwa wanafunzi wa Chuo hicho.Pia amesema kuwa wamejipanga vyema kuongeza miundombinu ilikukidhi mahitaji ya  Wanafunzi wapya wanaoongezeka kila mwaka chuoni hapo hasa Viti na Vyumba vya kusomea.

Rais wa Chuo hicho Ndg Eustard Rwegoshora(kushoto)Mkurugenzi Msaidizi wa Chuo hicho Bi Rahma Mohammed(katikati) na Katibu wa Chuo Ndg Ahmed Ngereza wakizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani)
Chumba Maalum cha Kompyuta
Maktaba ya Chuo hicho


No comments:

Post a Comment