HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 16 December 2013

"BREAKING NEWS" NA HABARI MPYA ZA KIMICHEZO KUTOKA LIGI KUU NCHINI UINGEREZA









AVB ATIMULIWA
LEO Tottenham imemfukuza kazi Meneja wao Andre Villas-Boas mara baada ya Jana kunyukwa Bao 5-0 na Liverpool.
Kipigo hicho cha Jana ndio kimekuwa kisago kikubwa kwa Timu hiyo kwa Miaka 16 Uwanjani kwao White Hart Lane na kimewaacha wakiwa Nafasi ya 7 kwenye Ligi Kuu England wakiwa Pointi 8 nyuma ya Vinara Arsenal.
 Villas-Boas, Miaka 36, aliteuliwa Meneja Tottenham Julai 2012.
Mwezi Machi 2012, Villas-Boas alifukuzwa kazi Chelsea baada ya kuwa hapo kwa Miezi minane tu.

Tottenham ilipigwa Bao 6-0 na Man City hapo Novemba 24 na, ingawa walitoka Droo na Mabingwa Man United na kuzifunga Fulham na Sunderland, kipigo hiki cha Liverpool kimewachukiza Wamiliki wa Klabu hiyo ambayo mwanzoni mwa Msimu ilimuuza Gareth Bale kwa Dau la Pauni Milioni 85 kwa Real Madrid, ikiwa ni Rekodi ya Dunia, na kununua msululu wa Wachezaji ambao ni Paulinho, Roberto Soldado, Nacer Chadli, Etienne Capoue, Christian Eriksen, Vlad Chiriches na Erik Lamela lakini Timu imekuwa ikifanya vibaya kwenye Ligi.

Hata hivyo, kwenye michuano ya Ulaya ya EUROPA LIGI, Tottenham imekuwa ikifanya vyema na kushinda Mechi zao zote 6 za Kundi lake na kutinga Raundi ya Mtoano ya Timu 32 ambako leo wamepangiwa kucheza na Dnipro, Klabu ya Ukraine.

Mbali ya mafanikio hayo, Villas-Boas pia ameipeleka Tottenham kwenye Robo Fainali ya Capital One Cup ambako Desemba 8 watacheza na West Ham.
Villas- Boas anakuwa Meneja wa 5 Msimu huu kutimuliwa kazi toka Klabu ya Ligi Kuu England wengine wakiwa Steve Clarke, aliefukuzwa Jana kutoka West Bromwich Albion, pamoja na Paolo Di Canio aliefukuzwa Sunderland Mwezi Septemba, Ian Holloway alitimuliwa Crystal Palace Mwezi Oktoba na Martin Jol aliepoteza kazi Fulham Wiki 2 zilizopita.

Wakati Huohuo
SERGIO AGUERO NJE MWEZI!
Kwa mujibu wa Meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini Nyota wao Sergio Aguero atakuwa nje kwa Mwezi mzima akiuguza Musuli za Mguu.
 
Aguero aliumia mapema Kipindi cha Pili hapo Jumamosi wakati City inaichapa Arsenal Bao 6-3.
Miongoni mwa Mechi muhimu ambazo Aguero atazikosa ni ile dhidi ya Liverpool lakini wapo wenzake, kina Alvaro Negredo, Edin Dzeko na Stevan Jovetic, ambao wanaweza kuziba nafasi yake.
MECHI ZINAZOFUATA ZA MAN CITY:
17 Desemba
Leicester v Man City
LC
21 Desemba
Fulham v Man City
LKE
26 Desemba
Man City v Liverpool
LKE
28 Desemba
Man City v Palace
LKE
1 Januari
Swansea v City
LKE
+++++++++++++++++++++++++++++++++

No comments:

Post a Comment