HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 22 November 2013

WAWILI WAOPOTEZA MAISHA AJALI ZA BARABARANI MKOANI TANGA


Kamanda Massawe

Na Gowdin Lyakurwa TANGA

Jeshi la Polisi Mkoani Tanga linamtafuta Dereva wa Gari namba T765 AXT aina ya Mitsubishi Fuso lililokuwa likitokea Korogwe kwenda katika kijiji cha Mgambo kwa kusababisha ajali iliyo pelekea kifo cha Mtu mmoja.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Cosntantine Massawe amesema kuwa tukio hilo limetokea Nov 21 mwaka huu majira ya saa 4:00 jioni katika barabara ya Korogwe- ambapo gari hilo likiendeshwa na dereva ambaye hajafahamika liliacha njia na akugonga mti ambao ulimuangukia mwendesha baiskeli alietambulika kwa jina la Mohammed Ally (28)Mkazi wa Mgambo na kufariki dunia hapo hapo.

 Kamanda Massawe amesema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa Dereva wa Gari hilo ambaye alikimbilia kusikojulikana baada ya tukio hilo.Mwili wa Mohammed umehifadhiwa Hospitali ya Wilaya ya Korogwe kwa uchunguzi zaidi na Jeshi la Polisi linandelea na upelelezi ili kumbaini na kumkamata Dereva huyo.

Wakati huohuo Jeshi la Polisi Mkoani hapa linamshikilia Hassan Juma (23) mkaazi wa kata ya kibirashi,Tarafa ya Mgera Wilaya ya Kilindi kwa kusababisha kifo cha Mtoto Salehe Sufiani(5) kwa kumgonga na pikipiki.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Costantine Massawe amesema kuwa tukio hilo limetokea mnamo Nov 21 mwaka huu majira ya saa 4:00 jioni katika kata ya kibirashi,Tarafa ya Mgera Wilaya ya Kilindi ambapo Hassani akiwa anaendesha pikipiki namba T 998 CCL alimgonga Mtoto Salehe Sufiani (5)mwanafunzi wa shule ya Kibirashi na kufariki hapohapo.

Chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi wa Pikipiki hiyo ambapo jeshi la Polisi linamshilikilia Mtuhumiwa kwa ajili ya kumchukulia hatua za kisheria.Mwili wa Mtoto huyo umekabidhiwa kwa ndugu zake baada ya kufanyiwa Uchunguzi.
Kufuatia matukio hayo kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Costantine Massawe ametoa wito kwa watumiaji wa Barabara kuwa makini na kuchukua taadhari wawapo barabarani hasa wakati wa Mwisho wa Mwaka.

No comments:

Post a Comment