HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Saturday, 16 November 2013

VITENDO VYA UBAKAJI, ULAWITI VYAKITHIRI MKOANI TANGA


Kamanda Massawe

Na Mwandishi Wetu Tanga
ZAIDI ya kesi za ubakaji 300 zimeripotiwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga katika kipindi cha Januari hadi Oktoba mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Costantine Massawe, alisema kati ya  kesi hizo 148 bado ziko kwenye upelelezi na 100 zinaendelea mahakamani ambapo 13 zilipata ushindi kwa washtakiwa kupatiwa adhabu ya mahakama.

Alieleza kesi tano zilishindwa mahakamani wakati 42 zilifungwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kutokuwa na ushahidi wa kuweza kupeleka kesi hizo kwa mwanasheria wa serikali kwa hatua za kisheria.

Kamanda  Massawe alisema a kwa upande wa makosa ya kulawiti 46 yaliripotiwa katika vituo vya polisi  mkoani hapa ambapo alisema kesi 18 ziko katika hatua ya upelelezi  wakati  16 zikiwa mahakamani na moja ilipata ushindi mahakamani na mshtakiwa kupatiwa adhabu  huku kesi moja ikishindwa mahakamani na 10 zikifungwa kutokana na sababu mbalimbali.
Kwa upande wa makosa ya kutupa watoto, manne yaliripotiwa ambapo kesi zote nne zilifungwa kutokana na sababu mbalimbali.

Aidha, Kamanda Massawe alisema jeshi la polisi mkoa wa Tanga kupitia Dawati la Jinsia na Watoto linaendelea kupokea kesi zinazojenga makosa ya jinai na zile ambazo zimekuwa na asili za makosa ya madai.

No comments:

Post a Comment