HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Saturday, 16 November 2013

HII NDIO JEURI YA PESSA "TAJIRI ATENGENEZA SHATI LA DHAHABU KUVUTIA WAREMBO"



 
Tajiri Datta Phuge akiwa amevaa shati late la dhahabu na vito vya thamani
Tajiri huyo, Datta Phuge mwenye umri wa miaka 32, alitumia sawa na shilingi milioni 35 kutengeneza shati la dhahabu tupu ili kuwavutia wanawake wampende.

Tajiri huyo aliwaajiri masonara 15 wamtengenezee shati hilo ambalo anaamini litawafanya wanawake wampapatikie kutaka kuolewa naye.

Tajiri huyo wa mji wa Pimpri-Chinchwad, ambaye biashara yake kubwa ni kutoa mikopo kwa watu, aliwaajiri masonara hao ambao walifanya kazi kwa masaa 16 kwa siku kwa muda wa wiki mbili ili kulitengeneza shati hilo ambalo limekamilika kila kitu pamoja na vifungo vyake vya dhahabu.

"Najua kuwa mimi sio mwanaume mwenye kuvutia sana lakini nina uhakika hakuna mwanamke ambaye hatapagawishwa na shati langu", alitamba Datta.

"Shati la dhahabu lilikuwa miongoni mwa ndoto za vitu nilivyotaka kuwa navyo", aliendelea kutamba tajiri huyo kijana ambaye ana uhakika wanawake wataanza kumpigia misele kutaka kuolewa naye.

No comments:

Post a Comment