HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 13 November 2013

"AIBU" BABU AMUOA MJUKUU JIJINI TANGA



 
Kamanda Costantine Massawe
Tanga.
 MZEE wa Miaka sabini anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kuoa binti mwenye umri chini ya miaka kumi na nane Mosa Hamisi kinyume cha sheria zilizopo hapa nchini.

Mkasa huo ulitokea Novemba 10 mwaka huu majira ya saa kumi na moja jioni ambapo mzee huyo tayari alishafunga ndoa na binti huyo lengo likiwa ni kuishi naye kama mke na mume.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga,Constatine Massawe amethibitisha kutokea tukio hilo na kueleza tayari jeshi linamshikilia mtuhumiwa huyo pamoja na mama mzazi wa binti huyo.

Massawe alimtaja mzee huyo kwa jina la Abdallah Tuppa (70)mkazi wa barabara kumi mbili na mama mzazi binti huyo Batuli Tupa (35)ambaye anaishi barabara kumi na nne jijini Tanga.

Alisema tukio hilo liligunduliwa na wasamaria wema baada ya kuona binti huyo anaozeshwa ndipo walipoamua kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ambapo wakati polisi walipofika eneo hilo walimkuta mzee huyo akidai mke wake ndipo walipomkamata.

Kamanda Massawe alisema askari walifanikiwa kumuhoji binti huyo ambapo alisema umri wake ni zaidi ya miaka kumi na saba hali ambayo ilipelekea kumuambia alete cheti chake cha kuzaliwa ili kuthibiti umri huo.

Wakati huo huo,mtu mmoja amekufa baada ya kugongwa na gari akiwa anaendesha baiskeli katika barabara ya Segera –Chalinze.

Kamanda Massawe alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 3 za usiku na kumtaja dereva aliyesababisha ajali hiyo kuwa ni Abdallah Msangi (30) wa gari hilo aina ya fuso lenye namba T390 DCB.

Massawe alimtaja aliyefariki katika ajali hiyo kuwa ni Hamisi Saidi mkazi wa Michungwani ambapo alisema chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva.

No comments:

Post a Comment